HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

August 13, 2019

SADC yajipanga kudhibiti biashara dawa za kulevya

NA SULEIMAN MSUYA

MKURUGENZI wa Sekretarieti ya Siasa, Ulinzi na Usalama  wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC),  Jorge Cardoso amesema jumuiya hiyo itashirikiana na nchi wanachama kukabiliana na biashara ya dawa za kulevya .

Akizungumza na waandishi wa habari leo Cardoso alisema wanatambua njia nyingi zinazotumiwa na waingizaji wa dawa za kulevya katika ukanda wa SADC, ikiwamo njia ya Pwani ya Kusini Mashariki mwa Afrika, ambazo wamekuwa wakishirikiana na Serikali za nchi husika kudhibiti uingizaji wa dawa hizo.

Alisema biashara ya dawa za kulevya ni tatizo kubwa na linaathiri nguvu kazi katika nchi wanachama ila wamekuwa wakifanya jitihada za makusudi kukabiliana na tatizo hilo.

 "Tumekuwa tukishirikiana na jumuiya ya kimataifa kuhakikisha tunadhibiti njia zote zinazotumika kuingiza dawa za kulevya katika nchi zetu,"alisema.

Mkurugenzi huyo alisema zipo njia za kuingiza dawa kutoka Amerika ya Kusini, Ulaya na kwingineko ila jambo la faraja ni kuwa wanapata taarifa kila kukicha.

Cardoso alisema wafanyabiashara wa dawa hizo wamekuwa wakibuni mbinu za kupata njia mpya kila wanapodhibitiwa, lakini wamekuwa wakishirikiana na jumuiya nyingine kukabiliana nao.

Aidha, alisema Polisi wa Kimataifa (Interpol) katika mkusimamia na kudhibiti bishara hiyo wamekuwa msaada mkubwa.

Alieleza kuwa wamekuwa pia wakishirikiana na vyombo vya Umoja wa Mataifa (UN) vinavyoshughulika na udhibiti wa dawa hizo.

Alisema kuhsu suala la demokrasia katika nchi wanachama, sekretarieti hiyo imeku ikisimamia na kuhakikisha viwango vinavyokubalika na nchi wanachama vinalindwa, kw akufuatilia taratibu zote za maandalizi, uchaguzi na baada ya uchaguzi kisha kutoa mapendekezo.

Alisema sekretarieti yake imekuwa ikisimamia masuala yanayohusu ushirikiano katika usalama pale yanapotokea majanga mbalimbali, kama ilivyotokea kwa kimbunga Idai, kilichosababisha maafa kwa zaidi ya watu 300,000 nchini Msumbiji, Malawi na Zimbabwe, ambao walihitaji misaada ya haraka.

Serikali ya Tanzania ilikuwa mstari wa mbele katika kutoa misaada ya halki na mali, ikiwamo misaada ya chakula na dawa kwa watu walioathiriwa na kimbunga hicho.

No comments:

Post a Comment

Pages