HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

September 08, 2019

VIONGOZI WATAKIWA KUCHUNGA NDIMI ZAO-MCHUNGAJI

Mchungaji wa Kanisa la Kinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Mtaa wa Ibura  Mchungaji Gabriel Lugakingira akiongoza ibada ya Jumapili.


Na Lydia Lugakila, Bukoba

Waumini wa madhehebu mbalimbali, viongozi wa dini  na viongozi wa serikali mkoani Kagera wametakiwa kujiadhali na matumizi  ya ndimi zao ili kuepukana  na kauli zinazoweza kusababisha migogoro isiyoisha.

Kauli hiyo imetolewa  leo  Septemba 8, 2019 na Mchungaji wa Kanisa la Kinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Mtaa wa Ibura  Mchungaji Gabriel Lugakingira katika ibada iliyofanyika kanisani hapo.

Mchungaji  Lugakingira ameendesha ibada hiyo kwa kuongozwa na  maneno ya mungu kutoka  Kitabu cha Mathayo mtakatifu  20, 20-23.

Mtumishi huyo amesema kuwa muumini yeyote kiongozi yeyote anayetoa kauli mbovu na kashifa ni chanzo kikubwa cha kuwepo kwa migogoro isiyoisha.

Amewataka kulifuata neno la mungu kwa kuchunga sana mdomo unaotoa kauli na kuwa mdomo unaweza kuunganisha watu na unaweza kufarakanisha  hivyo amesisitiza watu kujiadhali na matumizi mabaya ya ndimi zao.

‘’Dunia imeisha haribika vibaya watu wameshindwa kutumia Ndimi zao kila muhubiri anakuja na ndimi zake kwa waumini nyingine zikiwa za kashfa , zinazoeneza migogoro jiadhalini na mdomo  tubuni dhambi mtolee mungu shukrani ‘’amesema.

Amesema ulimi huo huo umesababisha hata kudharauliana kiimani na hata kuchochea  ubnafsi  huku akitaja sehemu ya stendi za mabasi kutumia ndimi zao vibaya .

Amesema jitihada za wanadamu zimeshindwa kuleta mafanikio dunia kutokana na ndimi zao hivyo amewahimiza kutoka katika  mitihani ya ibilisi na kufuata mitihani ya mwenyezi mungu.

Hata hiyo katika ibada hiyo yamefanyika maombi maalum kwa ajili ya kuwaombea wanafunzi wanaotarajia kufanya mthihani wa Darasa la saba.

No comments:

Post a Comment

Pages