HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

October 09, 2019

MAADHIMISHO YA MIAKA 145 YA SIKU YA POSTA DUNIANI, SHIRIKA LA POSTA LAKABIDHI ZAWADI KWA WASHINDI WA BARUA KIMATAIFA NCHINI

Mgeni rasmi, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Mawasiliano), Dkt. Jim Yonazi, akimkabidhi zawadi mshindi wa kwanza wa shindano la uandishi wa barua Kimataifa nchini, Joan John Erasto (wapili kushoto), wa Shule ya Sekondari Binza, mkoani Simiyu. Hafla ya maadhimisho ya miaka 145 ya Siku ya Posta Duniani imefanyika jijini Dar es Salaam leo. Kushoto ni mwalimu wa shule hiyo, Japhet Kilela.
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano wa Shirika la Posta Tanzania (TPC), Elia Madulesi akitoa maelezo katika hafla hiyo. Kulia ni Mgeni rasmi Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Mawasiliano), Dkt. Jim Yonazi. Wapili kulia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika, Dkt. Haruni Kondo.
Baadhi ya Maofisa wa Shirika la Posta Tanzania (TPC), wakifuatilia hotuba mbalimbali katika maadhimisho hayo. 
Kaimu Postamasta Mkuu wa Shirika, Mwanaisha Said, akizungumza katika hafla ya maadhimisho hayo. 
Mgeni rasmi Naibu Katibu Mkuu-Mawasiliano, Dkt. Jim Yonazi akimkabidhi zawadi  mshindi wa tatu wa uandishi wa barua, Hasnein Rizwan kutoka shule ya Sekondari ya Almuntazir Boys Seminary ya jijini Dar es Salaam.
Mgeni rasmi Naibu Katibu Mkuu (Mawasiliano), Dkt. Jim Yonazi akimkabidhi cheti mshindi wa pili wa shindano hilo, Grace Kahimba wa Shule ya Msingi ya St. Ann's ya Morogoro. Kulia ni Kaimu Postamasta Mkuu Mwanaisha Said na wa pili kushoto ni  Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika, Dkt. Haruni Kondo. 
Mshindi wa kwanza nchini katika shindano la Kimataifa la uandishi wa barua, Joan John Erasto, akiisoma barua yake iliyompatia ushindi wakati wa hafla hiyo.
Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Posta Tanzania, Dkt. Haruni Kondo akizungumza katika maadhimisho hayo, leo jijini.
Kaimu Postamasta Mkuu Mwanaisha Said, akimkaribisha  Mgeni rasmi, Naibu Katibu Mkuu (Mawasiliano), Dkt. Jim Yonazi (katikati), kuzungumza katika hafla hayo.
Mgeni rasmi Naibu Katibu Mkuu (Mawasiliano), Dkt. Yonazi  akizungumza katika maadhimisho hayo.
Mkurugenzi wa Kampuni ya Uwakala wa Usafiri wa ndege nchini (MAUFU), Maua Katandula, ambao ni mmoja wa wadhamini wa shindano la kimataifa la Uandishi wa Barua nchini, akizungumza katika maadhimisho hayo.
Mgeni rasmi Naibu Katibu Mkuu (Mawasiliano), Dkt. Jim Yonazi (katikati mbele waliokaa), akiwa katika picha ya pamoja na washindi wa shindano hilo, walimu, wazazi pamoja na wageni wengine waliohudhuria kwenye hafla hiyo.

No comments:

Post a Comment

Pages