HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

October 10, 2019

Sensei Kambi afariki Dunia

 Sensei Abdallah Kambi enzi za uhai wake.


 NA MWANDISHI WETU

MKUFUNZI na Mkuu wa Idara ya Ufundi ya JKA/WF Tanzania kitaifa, pia Mwenyekiti wa Tanzania Shotokan Ryu Karate Do Association (TASHOKA), Sensei Abdallah Kambi, amefariki Dunia.

Sensei Kambi aliyeingia madarakani Julai 27, 2019, amefikwa na umauti jana alfajiri katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, alipokuwa amelazwa kufuatia kusumbuliwa na kifua na tumbo, tangu Agosti mwaka huu.

Mwenyekiti wa JKA/WF Tanzania, Jerome Mhagama, amethibitisha kutokea kwa msiba huo na kwamba Sensei Kambi ambaye alijiunga na JKA/WF Tanzania mwaka 2009 na kuwa mwanafamilia hai mpaka umauti unamkuta.

Katika hatua nyingine, Mhagama alisema taarifa zaidi za msiba wa mdau huyo wa mchezo wa Karate, wanasubiri majibu ya kikao cha familia ya marehemu.

“Ndani ya JKA, Kambi Sensei alikuwa mmoja wa Wakufunzi tegemezi mwenye Mkanda Mweusi Dani 4 ‘Black Belt 4th Dan-­‐JKA’, pia alikuwa na leseni ya kimataifa ‘JKA International License’ yenye viwango vya ‘Instructor class C’, ‘Judge class D & Examiner class D’”, alisema Mhagama katika taarifa yake kwa vyombo vya habari jana.
Mungu ailaze mahala pema roho ya maremu. Bwana ametoa, Bwana ametwaa, jina lake lihimidiwe.

Alale mahali pema peponi..!

No comments:

Post a Comment

Pages