HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

October 10, 2019

TMA YATOA MWELEKEO WA HALI YA HEWA KWA MAENEO YANAYOPATA MVUA ZA MSIMU MMOJA KWA MWAKA

 Mkurugenzi wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), Dk. Agnes Kijazi, akitoa mwelekeo wa hali ya hewa kwa maeneo yanayopata mvua za msimu mmoja kwa mwaka kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) jijini Dar es Salaam. (Na Mpiga Picha Wetu).
 Mkurugenzi Dk. Agnes Kijazi, anazungumza akizungumza na waandishi wa habari wakati akitangaza mwelekeo wa mvua za msimu kwa maeneo yanayopata msimu mmoja wa mvua kwa mwaka. Kulia ni MKurugenzi wa TMA, Dk. Hamza Kabelwa na kushoto Meneja Kituo Kikuu cha Utabiri TMA, Samwel Mbuya.


Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa rasmi utabiri wa msimu wa mvua za mwaka (Novemba 2019 hadi Aprili 2020) na athari zinazoweza kujitokeza. Utabiri huo ni mahususi kwa maeneo yanayopata mvua mara moja kwa mwaka ikiwa ni mikoa ya Kigoma, Tabora,Rukwa,Katavi,Mbeya, Songwe, Njombe,Iringa, Lindi, Dodoma, Singida, Mtwara na Kusini mwa mkoa wa Morogoro.


Akizungumza na waandishi wa habari, Mkurugenzi Mkuu wa TMA na Makamu wa tatu wa Rais wa WMO Dkt. Agnes Kijazi aliwataka wananchi wa maeneo hayo kuzitumia vizuri mvua hizo kwa kupata ushauri kutoka kwa wataalamu wa sekta husika kwa vile maeneo mengi yanatarajiwa kuwa na mvua za kutosha. ‘Naendelea kutoa rai kwa wananchi wa mikoa husika kuzitumia mvua hizi kwa kupanda mazao sahihi kwa kufuata ushauri wa wataalamu, kama tunavyoona maeneo mengi yatarajiwa kuwa na mvua za juu ya wastani hadi wastani’, alisema Dkt. Kijazi.


 Aidha, Dkt. Kijazi alifafanua kuhusu mvua zinazoendelea kunyesha kwa maeneo ya kaskazini mwa nchi kwa kusema kuwa mvua hizi ni za msimu wa vuli kwa maeneo yanayopata mvua mbili kwa mwaka na katika kipindi hiki cha vuli kunatarajiwa kuwa na vipindi vifupi vya mvua kubwa ambapo alimalizia kwa kuwataka wananchi kuendelea kufuatilia taarifa za hali ya hewa zinazotolewa na TMA sambamba na kuchukua tahadhari ya vipindi vifupi vya mvua kubwa,upepo mkali na mawimbi makubwa, vinavyotarajiwa kujitokeza katika baadhi ya maeneo.

Utabiri uliotolewa kwa maeneo yanayopata mvua za msimu mara moja kwa mwaka unaonesha maeneo ya mengi ya mikoa ya Dodoma, Singida, Tabora, Mbeya, Songwe, Ruvuma, Njombe, Iringa, Rukwa Kusini mwa mkoa wa Morogoro, Lindi na Mtwara, yanatarajiwa kupata mvua za juu ya wastani hadi wastani na maeneo ya mikoa ya Kigoma na Katavi, yanatarajiwa kupata mvua za wastani hadi juu ya wastani.

No comments:

Post a Comment

Pages