HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

January 25, 2020

DC Hanang; Ubinafsi, Siasa za Makundi vilidumaza Elimu


Wanafunzi na Walimu wa Sekondari ya Balang’dalalu Wilaya ya Hanag.
Na Bryceson Mathias
 
MKUU wa Wilaya ya Hanang mkoani Manyara, Joseph Mkirikiti, ameonya Ubinafsi na Siasa za Makundi, ni Msumari wa Moto uliochelewesha Maendeleo ya Elimu wilayani humo, na kujigamba kupitia Mchango wa Serikali ya Awamu ya Tano, Elimu sasa inashika Kasi!.
Mkirikiti alisema hayo alipohojiwa juu ya Kilio cha Wananchi kuhusu Changamoto za Miundombinu Mibovu ya Majengo, Maabara na Upungufu wa Walimu wa Sekondari Kongwe ya Bweni ya Balang’dalalu ambayo 2019/2020 Kidato cha Nne na Pili ilifanya vizuri ikiwa na Div 1=14, II=23, III=19, IV=19, na 0=6, ambapo Mwandishi hakuuruhusiwa kupiga picha ya majengo hayo kwa madai kuna Katazo!!
Akifafanua alisema, hili si kificho tangu niingia hapa 2018 kwa msaada wa  Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM), John Magufuli, na Katibu Mkuu, Ally Bashiru, kazi ilikuwa ni kuvunja makundi ya kisiasa baina ya, Mary Nagu, na Waziri Mkuu Mstaafu, Fredrick Sumaye, ili kuleta Umoja, ambayo yalikwamisha ihata Maendeleo ya Elimu.
“Miongoni mwa wana Umoja wa wana Hanang in Dar walipotaka kurudi kwao kuja kuchangia Maendelo, walionekana kana kwamba wanataka kuja kugombea Ubunge au Udiwani, hivyo kile walichokuwa nacho kwa ajili ya kuchangia maendeleo ya Miundo Mbinu na Elimu walishindwa kuepuka maneno.
“Tunaishukuru Serikali kupitia kwa Rais Magufuli, Waziri wa TAMISEMI na Katibu Mkuu wake, walitoa Mil. 115 ambazo zimejenga Hostel na Halmashauri ya Hanang iliyotoa Mil.20 ambazo zimemalizia ili wakitusaidia tukarabati Mabaara”.alisema Mkirikiti
Diwani wa Kata hiyo, Paulo Tsaxara, alisema Sekondari ya Balang’dalalu ilikuwa ya Kanisa la Kiinjilili la Kilutheri Tanzania (KKKT) tangu 1988 ikachukuliwa na Serikali, nakiri Miuundo Mbinu yake ni mibovu na ina Walimu wachache maana ilisahauliwa, lakini kwa sifa ya ufaulu iliyonao ikumbukwe!.
“Mbali ya Ubinafsi na Makundi ya Kisiasa, chnagamoto nyingine ni wenyeji kuona sekondari hiyo kama siyo yao kwa sababu walipoomba pia iwe na Wanafunzi wa Kutwa ili wenyeji Watoto wao wasome! Haikukubalika kwa wanafunzi wengi wanatoka nje” alisema Diwani Tsaxara alyesema alisoma shule hiyo ikiwa ya msingi 1973.
Diwani Tsaxara, ameiomba tena Serikali na Viongozi waliosoma shule hiyo wakiwemo, waliowahi kuwa Wakuu wa Wilaya nchini, Majaji, Viongozi wa dini ikiwemo KKKT, Waandishi (akimtaja, Zephaniah Ubwani, na yeye), kuikumbuka shule hiyo iliyo na maabara mbovu na walimu wachache jiapo wanafanya kazi nzuri, iweze kukarabatiwa maana mabati yake yenye kuoza ni ya 1988.

No comments:

Post a Comment

Pages