HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

January 26, 2020

Mzumbe yawapa wanafunzi mbinu za kujiajiri

Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Mzumbe, Prof. Lugano Kusiluka, akizungumza wakati wa kongamano la vijana wanaosoma vyuo mbalimbali nchini lililoandaliwa na chuo hicho ambalo linafahamika kama (TESCEA), kitengo cha huduma za ajira, kinachowaunganisha watafuta kazi na mwajili.
 Baadhi ya wanafunzi walioshiriki kongamano hilo.
 Picha ya pamoja.


Na Ghisa Abby

CHUO Kikuu Mzumbe kimeandaa mradi maalumu utakaowawezesha wahitimu kutoka vyuoni kuweza kujiajiri, kuajirika na kutafuta fursa za kuanzisha biashara.    

Makamu mkuu wa chuo kikuu Mzumbe Profesa Lugano Kusiluka alizungumza hayo wakati wa kongamano la vijana wanaosoma katika vyuo mbalimbali nchini lililoandaliwa na chuo hicho ambalo linafahamika kama (TESCEA) kitengo cha huduma za ajira, kinachowaunganisha watafuta kazi na mwajiri.

Alisema lengo la kuanzisha mradi huo ni kuzalisha wahitimu wenye elimu, ujuzi na nia kuwawezesha wahitimu kutoka vyuo mbalimbali kuweza kujiajiri na kupata fursa za kuajiliwa. 

Aidha Profesa Kusiluka alisema kuwa chuo hicho kimetumia wawezeshaji kutoka katika taasisi za serikali kuweza kuwafundisha vijana waliopo kwenye vyuo vikuu mbalimbali lengo likiwa kuwaona vijana hao wanapata msaada na kupata fursa zinazotolewa na serikali ikiwemo mikopo.

Aidha Kusiluka aliwataka vijana kuacha kutegemea kuajiriwa peke yake bali wawe wabunifu na kujiajiri.

Kwa upande wake Mwezeshaji kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu, Mitengo cha Kazi, Vijana, Ajira na Watu Wenye Ulemavu, Nassibu Mwaifunga alisema kuwa mfuko wa maendeleo ya vijana umeanzishwa na serikali lengo likiwa kuwawezesha vijana kuweza kupata mitaji.

Alisema kupitia kongamano hilo serikali ina lengo la kuona vijana wengi kutoka vyuo vikuu wanaweza kutumia fursa zilizopo ili kuweza kujiajiri na kuondoa mawazo ya kuweza kuajiriwa.
Mkurugenzi Kitengo cha Huduma za Ajira, Joseph Nganga alisema kuwa kongamano hilo ni muhimu kwani chuo hicho kimeona namna kuwawezesha vijana kwendana na soko la ajira.
Pia Serikali inatekeleza mpango muhimu wa wahitimu kutoka vyuo vikuu vyote nchini kwenda kufanya kazi kwa muda wa mwaka mmoja kwa mwajili ya kupata ujuzi wa taaluma aliyonayo kabla ya kuajiriwa.
Aidha, amewataka vijana wote wanaohitimu kutoka vyuo vikuu kote nchini kutumia fursa kutoka kitengo huduma za ajira kupata mafunzo yakuweza kuajirika.

Katibu Mtendaji Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC),  Bengi Issa alisema kuwa kama baraza linasimamia ujasiriamali na kuhakikisha somo lake linafundishwa kwenye vyuo vyote nchini.

Alisema pia wanatengeneza mikakati jinsi ya uwezeshaji kwa wananchi kujikomboa hasa vijana, wanawake kufikia uchumi wa kati.  

Baadhi ya wanafunzi walioudhuria kongamano hilo akiwemo Magdalena wa Mzumbe, alieleza kuwa wanashukuru uongozi wa chuo kutatua changamoto ya kutembea na bahasha mkononi kutafuta ajira pindi wanapohitimu masomo yao bali watatumia fursa hiyo kuweza kuwaelimisha na wenzao.

No comments:

Post a Comment

Pages