HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

February 19, 2020

Tigo waja na ‘Toa bei na Ushinde’

Mtaalam wa Huduma za Kidigitali za Tigo, Ikunda Ngowi, akizungumza wakati akitangaza promosheni maalumu ijulikanayo kama‘Toa bei na Ushinde’ au Bid-2-Win kwa ajili ya wateja wa kampuni hiyo.


 Na Mwandishi Wetu

KAMPUNI ya Simu ya Tigo Tanzania  imekuja na promosheni ijulikanayo kama‘Toa bei na Ushinde’ au Bid-2-Win.

Akitangaza promosheni hiyo jijini Dar es Salaam Mtaalam wa Huduma za Kidigitali za Tigo, Ikunda Ngowi alisema promosheni hiyo ni maalumu kwa ajili ya wateja wa Tigo ikiwa ni sehemu ya kuonesha shukrani zao kwa kuendelea kuwaamini na kutumia mtandao huo.

“Promosheni hii inatoa nafasi kwa wateja kununua bidhaa mbalimbali kwa bei ya chini au pungufu.Katika promosheni hii wateja wateweza kujishindia zawadi zenye thamani ya hadi shilingi milioni 5.

Kimsingi, ‘Toa bei Ushinde’ ni huduma ambayo inampa nafasi mteja kushinda bidhaa aipendayo kila wiki kila anaposhiriki kwa kutaja bei ambayo anaweza kununua bidhaa hiyo,” alisema.
Mtaalam huyo alisema zawadi hizo zinahusisha bidhaa za kisasa na za kibunifu zikiwemo simu janja aina ya Samsung A30, A70, A50, Home internet routers pamoja na Playstations aina ya Sony ambapo bei ya chini ya kuanzia ni shilingi 1000.

“Tunafurahi kuzindua rasmi promosheni hii na tunaamini kuwa itawapa nafasi wateja wa Tigo kupata bidhaa za kidigitali kwa gharama nafuu, huduma hii ni ya haki na inampa kila mteja nafasi ya kushinda zawadi mbalimbali kulingana na thamani yake,” aliongeza.

Alisema kama kampuni ya kidigitali, wanatambua mahitaji ya wateja wao ndio maana siku zote wapo mstari wa mbele kuleta suluhisho zenye kuboresha namna watu wanavyotumia huduma za mawasiliano.
Ngowi alisema huduma hii inamruhusu mteja kutoa bei ya bidhaa husika na kumpa nafasi ya kushinda bidhaa hiyo. “Tunaamini kupitia promosheni hii tutafungua njia kwa Watanzania wengi kutumia teknolojia za kidigitali,” alisema.
Alisema ni imani yao kuwa, huduma hiyo itapungumza makali ya bei za bidhaa na kuwapa nafasi wateja kumiliki bidhaa wazipendazo kwa gharama nafuu kwa urahisi zaidi kupitia Tigo.
Alisema Tigo imekuwa mstari wa mbele kuleta mapinduzi ya kidigitali ikiwamo kuanzisha huduma ya
Simu janja (Smartphone) ya Kiswahili, Facebook ya bure, App ya Tigo Pesa na zaidi kuwa kampuni ya Kwanza kutoa huduma ya kutuma na kupokea pesa katika nchi za Afrika Mashariki.

“Ni imani yetu kuwa, Huduma hii pia itapungumza makali ya bei za bidhaa na kuwapa nafasi wateja kumiliki bidhaa wazipendazo kwa gharama nafuu kwa urahisi zaidi kupitia Tigo.

Hivyo basi, tunawahimiza wateja wetu kushiriki kwa wingi katika promosheni hiyo kwani kadiri unavyoshiriki ndivyo unavyojiweka katika nafasi nzuri zaidi ya kushinda.

Ili kushiriki mteja wa Tigo anaweza kutuma ujumbe mfupi meseji wenye neno BID kwenda 15371.Kila meseji itatozwa kiasi cha shilingi 50 na washindi watapatikana kila wiki,” alisema.

No comments:

Post a Comment

Pages