HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

March 05, 2020

KILIMANJARO PREMIUM LAGER MFANO WA KUIGWA-

Mkurugenzi wa Masoko TBL, Doreen Tumubeebire (kushoto) na Meneja wa Bia ya Kilimanjaro Premium Lager, Irene Mutiganzi wakiteta jambo huku wakifuatilia mbio za Kilimanjaro Premium Lager Marathon 2020 zilizofanyika Mjini Moshi hivi karibuni.



Na Mwandishi Wetu

 SHIRIKISHO la Riadha Tanzania (RT), limeipongeza kampuni ya Bia Tanzania (TBL), kupitia kinywaji chake cha Kilimanjaro Premium Lager kwa mchango wao uliotukuka katika uhai wa mbio maarufu za Kilimanjaro Marathon.

Mbio za Kilimanjaro Marathon zilifanyika Machi Mosi mwaka huu, Moshi mkoani Kilimanjaro zikiwa zinatimiza miaka 18 tangu kuanzishwa kwake.

Akizungumzia mbio hizo, Makamu wa Kwanza wa Rais RT-Utawala, William Kallaghe, ambaye alimwakilisha Rais wa shirikisho hilo, Anthony Mtaka, alisema mbio hizo hivi sasa zimekuwa kubwa na nembo ya Taifa, lakini hasdi kufikia hapa Bia ya Kilimanjaro Premium Lager inapaswa kupongezwa, kwani imekuwa mdau mkubwa kwa miaka yote hiyo.

“Sekta ya michezo ni vigumu kupiga hatua bila udhamini, sisi kama Shirikisho la Riadha Tanzania (RT), tunapenda kupigia mfano udhamini mfululizo wa Kilimanjaro Premium Lager, kwani wamekuwa na mbio hizi kwa miaka yote hiyo bila kusimama,” alisema Kallaghe na kuongeza. Huu ni udhamini wa kipekee na kuigwa na wadhamini wengine.
 
Kallaghe, alisema Kilimanjaro Premium Lager Marathon, sasa limekuwa ni tukio kubwa nchini lenye kugusa mataifa mbalimbali, ambayo washiriki wake wamekuwa wakivutika kushiriki mwaka hadi mwaka huku akiongeza kuwa tukio hili linatakiwa kuwa la kitaifa na sio la Moshi tu.

Aliwaomba wadhamini wengine, kuzidi kujitokeza kuwekeza kwenye mchezo wa riadha, ambao hivi umekuwa na mvuto kwa watu wengi nchini.

Naye Mwenyekiti wa Chama cha Riadha Mkoa wa Kilimanjaro (KAAA), Liston Metacha, alisema kama mkoa wanajivunia kuwa na tukio kubwa kama hilo na wakidumu nalo kwa miaka 18 bila kukoma.

Metacha, alisema Kilimanjaro Marathon imekuwa na mchango mkubwa kimichezo na kiuchumi sit u kwa Mkoa wa Kilimanjaro, bali Tanzania kwa ujumla hususan kupitia sekta ya utalii. 

Mwenyekiti huyo, aliwaomba Kilimanjaro Premium Lager na wadhamini wengine ikiwamo kampuni ya simu ya Tigo, kuendelea kuliunga mkono tukio hilo la kila mwaka.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Masoko TBL, Doreen Tumubeebire, alisema wanajisikia furaha mbio kila mwaka inakua na hadi sasa inapofikisha miaka 18 wamefikisha washiriki zaidi ya 11,000.

“Hii inaonyesha jinsi gani watu wametambua umuhimu wa michezo, na katika kuimarisha afya zao,” alisema Doreen na kuongeza mwaka huu wametumia zawadi Sh. Milioni 23 huku Mtanzania wa kwan za katika mbio za Kilomita 42 wanaume na wanawake amepata Sh. Milioni 1.5 kama bonasi.

Mbio za mwaka huu, zimewezeshwa na Kilimanjaro Premium Lage-42km, TIGO-21km, Grand Malt-5km, Maji ya Kilimanjaro, TPC Limited, Simba Cement, Unilever, Absa Bank Tanzania Limited wakati wadhamini wa huduma ni Kibo Palace Hotel, Keys Hotel, GardaWorld Security, Precision Air, CMC Automobiles.

No comments:

Post a Comment

Pages