DAR ES SALAAM, TANZANIA
NGULI
wa habari na mtangazaji mahiri wa Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC), Marin
Hassan Marin (pichani), aliyefariki dunia leo Aprili 1, jijini Dar es Salaam, anatarajia
kuzikwa kesho Alhamisi Aprili 2 kwenye Makaburi ya Mwanakwerekwe, visiwani
Zanzibar.
Marin
Hassan, amefariki dunia leo Aprili 1, 2020 katika Hospitali ya Jeshi Lugalo,
Dar es Salaam, alikokimbizwa na majirani baada ya kulalamika kutojisikia vema
mapema leo asubuhi. Taarifa za kifo chake, zilithibitishwa na Kaimu Mkurugenzi
Mkuu wa TBC, Martha Swai.
Mkongwe
huyo aliyezaliwa mwaka 1972, alikuwa jijini Dar es Salaam katika uzinduzi wa
kipindi chake cha Ardhio cha TBC1, uliofanyika Machi 30, kabla ya kushiriki
kipindi hicho Machi 31, ambako aliondoka studio za TBC Mikocheni akiwa mzima wa
afya saa 3:30 usiku.
Rais
John Magufuli, ametuma salamu za rambirambi kwa TBC na familia ya marehemu
Marin, ambako ametoa ndege binafsi ya Rais, iliyofuata baadhi ya wana familia
mjini Dodoma, kisha kwenda Dar es Salaam kuchukua mwili wa marehemu kuupeleka Zanzibar
kwa maziko.
Habari
kutoka nyumbani kwa marehemu Kibweni mjini Zanzibar, zinaeleza kuwa mipango ya
maziko inafanyika na mazishi ya nguli huyo yanatarajia kufanyika Alhamisi,
Aprili 2, majira ya saa 4 asubuhi, kabla ya sala ya Adhuhur, huko Mwanakwerekwe.
No comments:
Post a Comment