HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

June 03, 2020

MAWAKALA BENKI WANAOKATAA FEDHA ZA MALIPO YA WAJASIRIAMALI KUCHUKULIWA HATUA

Mkuu wa Wilaya ya Nzega Godfrey Ngupula akitoa ufafanuzi jana kwa Watendaji wa Vijiji na Kata wakati walipokuwa wakielezwa umuhimu wao kusimamia zoezi la ugawaji wa Vitambulisho vya Wajasiriamali.
Kaimu Meneja wa Mamlaka ya Mapato nchini (TRA) Mkoani Tabora Aniseti Antony akieleza jana wilayani Nzega aina ya wafanyabiashara wadogo ambapo wanapaswa kuchukua vitambulisho.


NA TIGANYA VINCENT


SERIKALI Mkoani Tabora inachunguza tuhuma dhidi ya baadhi ya Mawakala wa Benki  ambao wanakataa kupokea fedha za vitambulisho vya wajasiriamali wadogo kwa madai hawapati faida.

Kauli hiyo imetolewa jana wilayani Nzega na Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri baada ya kupata malalamiko kutoka kwa Watendaji kuwa Mawakala wa Benki wanakata kupokea fedha zinakusanywa kutoka kwa Wajasiriamali wadogo.

Alisema wakiwabaini Mawakala ambao wamekataa kupokea fedha itawasaliana na Benki husika ili ziweze kuchukua hatua dhidi ya Mawakala hao.

Mwanri alisema kuwa maelekezo ya Seikali yako wazi kuwa fedha zote zitalipwa kwa kutumia Control Number kupitia Wakala wa Benki au Benki na sio vingine.

Alisema watakaobainika kuwa wanaokataa kupokea fedha kwa madai hawapati faida watahesabiwa kuwa wanahujumu jitihada za Serikali na watachukuliwa hatua ili iwe fundisho kwa wengine.

Mkuu huyo wa Mkoa aliongeza hairusiwi Watu wote waliopewa jukumu la kugawa vitambulisho kwa wajasiriamali wadogo kutumia fedha kwa kutumia mitandao ya simu.

Alisema kufanya hivyo kutasababishia Serikali kupata fedha pungufu ya gharama halisi ya kitambulisho na hivyo kuzalisha hoja.

Kwa upande wa Kaimu Meneja wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoani Tabora Aniseti Antony alisema Mamlaka hiyo ina mkataba ya Benki , hivyo inasikitishwa na kitendo cha Wakala wao kukata kupokea fedha za vitambulisho.

Alisema Serikali ina utaratibu wake wa kuzilipa Benki . hivyo Mawakala hawapaswi kugoma kupokea fedha za Vitambulisho.

Antony alisema watajitahidi kuwasiliana na Benki husika ili kuhakikisha zoezi hilo halikwami na kusababisha Watendaji kukaa na fedha za umma kwa muda mrefu bila kuziwasilisha Benki.

No comments:

Post a Comment

Pages