HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

June 03, 2020

RC TABORA KUWACHULIA HATUA WATENDAJI WATAKAO TUMIA FEDHA ZA KATIKA BIASHARA ZAO

Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri akitoa elimu leo kwa Wafanyabiashara wadogo wa Puge wilaya Nzega juu ya umuhimu wa kuchukua vitambulisho vya Wajasiriamali. (Picha na Tiganya Vincenti).


NA TIGANYA VINCENT

SERIKALI imesema itawachukulia hatua Watendaji ambao wataobainika kuzungusha fedha za vitambulisho vya Wajasiriamali wadogo kwa nia ya kutaka kuzalisha faida kabla ya kuzikabidhi Benki.

Kauli hiyo imetolewa jana wilayani Igunga na Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri wakati akiendesha zoezi la kuwahamasisha wajasirimali kuchukua vitambulisho vipya vilivyotolewa hivi karibuni na Serikali.

Alisema kuna tabia ya baadhi ya Watendaji wanaweza kukusanya fedha za vitambulisho na kuzipangia matumizi yao binafsi kwa lengo kuwa wakishazalishi ndio wapeleke Benki.

“Ni marufuku kutumia fedha za viparata ili kuzungushia kwenye biashara zenu mnaweza kupoteza fedha za umma na kujikuta katika matatizo…mkichukua fedha hizo mkaenda kununua ng’ombe au mkanunua mpunga kwa lengo la kutaka kuzalisha mtajikuta mnajiingiza katika matatizo na kushitakiwa na kufukuzwa kazi” alisisitiza.

Mwanri alisema Mtendaji yoyote atakayekuwa ametumia fedha hizo atahesabika kuwa mwizi na kupelekwa Mahakamani kwa kosa la wizi wa fedha za umma.
Naye Kaimu Maneja wa Mamlaka ya Mapato Tanzania(TRA) Mkoani Aniseti Antony alisema matumizi ya fedha za umma yanautaratibu wake.

Alisema ni marufuku kutumia fedha za umma kabla ya kuidhinishwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

No comments:

Post a Comment

Pages