HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

June 01, 2020

RC TABORA ATOA MWEZI MMOJA VITAMBULISHO VYOTE VIWE VIMEKWISHA

NA TIGANYA VINCENT

MKUU  wa Mkoa wa Tabora, Aggrey Mwanri, ametoa mwezi mmoja kwa viongozi wa Halmashauri zote kuhakikisha wamemaliza kugawa vitambulisho vya wajasiriamali ambavyo vimetolewa hivi karibuni.

Alisema hakuna sababu ya kuchukua muda mrefu katika ugawaji wa vitambulisho hivyo kwa sababu wameshapata uzoefu kutokana na vile vya mwaka jana.

Mwanri alitoa kauli hiyo jana mjini Igunga wakati wa mkutano wake na Watendaji wa Kata na Vijiji kuhusu umuhimu wa kutekeleza zoezi hilo.

 Alisema uendaji wa Mtendaji yoyote utapimwa pamoja na majukumu mengine ni pamoja na jinsi aakavyofanikisha zoezi la kuwezesha wajasirimali wadogo na watoa huduma kuchukua vitambukusho

Aidha Mwanri aliongeza kuwa kila watakapokuwa wakiuza kitambulisho wahakikishe fedha wanazipeleka benki au wanalipa kwa wakala wa Benki kwa kutumia Control namba.

Katika hatua nyingine Mkuu huyo wa Mkoa ametahadharisha Waendaji kuwa makini kabla ya kutoa vitambulisho kwa kupata taarifa sahihi ya mhusika ili kuhakikisha wanaopatiwa ni walengwa tu na sio wafanyabiashara wakubwa.

Alisema kuna uwezekano wa Wafanyabiashara wakubwa wakatumia wafanyabiashara wadogo kuchukua vitambulisho hivyo kwa ajili ya kukwepa kodi.

No comments:

Post a Comment

Pages