HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

June 04, 2020

RC TABORA NZEGA DC KUANZA KUKATA MISHAHARA YA WATUMISHI WANAODAIWA MASURUFI

  Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri(katikati) akikabidhi jana mfano wa hundi yenye thamani ya shilingi milioni 140 kwa vikundi mbalimbali vya Halmashauri ya Mji wa Nzega. (Picha na Tiganya Vincent).

 
NA TIGANYA VINCENT


UONGOZI wa Halmashauri ya Wilaya ya Nzega umeagizwa kukata katika mishahara watumishi wanaodaiwa masurufi ya kiasi cha shilingi milioni 10.3 yaliyosababisha hoja ya kiukaguzi kutoka kwa Mdhibiti wa Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG).
Agizo hilo Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Aggrey Mwanri, ameagiza kuwakata mishahara watumishi wote wa alilitoa wakati wa kikao maalumu cha Baraza la Madiwani la Halmashauri hiyo la kupitia hoja ya mbalimbali  kutoka ripoti ya ukaguzi ya CAG kwa mwaka 2018/19.
Alisema ndani ya mwezi mmoja watumishi wote wanaodaiwa wahakikishe wamelipa fedha hizo au wakatwe kwenye mishahara yao.
Mwanri alisema wasipo katwa fedha hizo hoja hiyo itaendelea kujitokeza na kuchafua hesabu za Halmashauri hiyo wakati wa ukaguzi wa CAG.
Aliwataka  Wakuu wa Idara kuhakikisha wamefanyia kazi hoja zote za CAG na kuwalisilisha vielelezo ili ziweze kufungwa.
Alisema watumishi ni vema wakajitahidi kuzuia hoja na zio kutoa maamuzi ambayo yanasababisha kuendelea kuzalisha hoja kila mwaka.

Katika hatua nyingine Mkuu wa Mkoa amemwagiza Katibu Tawala Msaidizi(Serikali za Mitaa) kushirikiana na Mkurugenzi Mtendaji , Meneja wa RUWASA kuhakikisha wanaibana Drilling Ltd irejeshe shilingi milioni 23.5 baada ya kuchimba visima ambavyo havikuwahi kutoa maji.

Alisema fedha hizo zilipaswa kuwa zimerejeshwa tangu mwaka jana mwezi Septemba ambapo hadi hivi sasa hakuna fedha zilizorejeshwa na kuongeza kuwa ikiwa itashindwa kurejesha waipeleke Mahakamani.

No comments:

Post a Comment

Pages