HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

June 04, 2020

NZEGA MJI YATOA MIKOPO YA SHILINGI MILIONI 14O KWA VIKUNDIKULIWA HATUA

Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri akizungumza na Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Nzega wakati wa kikao cha kupitia taarifa ya ukaguzi kutoka katika Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG).



NA TIGANYA VINCENT


HALMASHAURI  ya Mji wa Nzega imetoa jumla ya shilingi milioni 140 kwa vikundi 40 ikiwa ni sehemu ya asilimia 10 ya mapato ya ndani.

Mikopo hiyo imekabidhiwa kwa vikundi  hivyo katika  halfa fupi ilifanyika jana mjini Nzega.

Akizungumza wakati wa kukabidhi, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo Philemon Magesa alisema kuwa vikundi 24 vya wanawake vimepatiwa mikopo ya shilingi milioni 74.5.

Aliongeza kuwa kwa upande wa vikundi 11 vya vijana vimekopeshwa shilingi milioni 38 na vikundi 5 vya watu wenye ulemavu vimekopeshwa shilingi milioni 27.5. 

Wakati huo huo Magesa alisema kuwa katika kipindi cha mwezi Januari mwaka huu walitoa mikopo ya shilingi milioni 70 kwa vikundi mbalimbali.

Akizungumza baada ya kukabidhi mikopo hiyo kwa niaba ya Halmashauri hiyo, Mkuu wa Mkoa Aggrey Mwanri aliutaka uongozi wa Halmashauri hiyo kuhakikisha wanatoa elimu ya kutosha kwa wakopaji ili waweze kutambua umuhimu wa kurejesha fedha hizo kwa wakati.

Alisema hatua hiyo itavisaidia vikundi kutumia fedha kwa malengo waliyoombea na sio katika shughuli nyingine ikiwemo starehe na kuwafanya washindwe kulipa kwa wakati.

Mwanri alisema hatua hiyo itawasaidia kuepuka kuwa na wadaiwa ambao wanawasababisha kupata hoja za Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali(CAG) ambazo zinatokana na fedha ambazo hazijarejeshwa.

Aidha Mkuu wa Mkoa aliushauri uongozi wa Halmashauri hiyo kuangalia uwezekano wa kuvikopesha vikundi vifaa vitakavyosaidia kuanzisha viwanda vidogo vodogo.

Katika hatua nyingine Mkuu wa Mkoa huyo ameagiza uongozi wa Halmashauri ya Mji wa Nzega kuhakikisha milioni 22.6 zilizokopeshwa katika vikundi mbalimbali zinarejeshwa ili kufuta hoja za kiukaguzi.

Alisema ni vema wakasaliana na wahusika ili waonyeshe mpango wao wa kulipa deni na wakishindwa kurejesha kwa hiari wahakikishe wanapeleka Mahakamani

No comments:

Post a Comment

Pages