HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

June 08, 2020

WAKULIMA NA WAFUGAJI WATAKIWA KUDUMISHA UPENDO NA USHIRIKIANO

 Mdau wa maendeleo, Brighton Armi, akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kukabidhi msaada wa vitu mbalimbali kama mashine za kunawihia mikono, vitakasa mikono na ndoo maalum za kunawa kwa uongozi wa kijiji cha Malolo kilichoko wilaya ya Kilosa.
 Mdau wa maendeleo, Brighton Armi, akimkabidhi afisa mtendaji wa kijiji, Ferdinand Weteka  baadhi ya vitu alivyokabidhi kwa ajili ya kituo kipya cha afya cha kijiji cha Malolo na shule za msingi na sekondari za kijiji hicho.


Na Denis Mlowe, Kilosa

JAMII ya wafugaji na wakulima nchini wametakiwa kudumisha upendo na ushirikiano kuepusha migogoro ya mara kwa mara kwa lengo la kudumisha amani katika maeneo wanayoishi.

Ushauri huo umetolewa na mwanajamii  mfugaji ,Brighton Armi mdau wa maendeleo ambaye anasoma nchini Ujerumani wakati akikabidhi msaada wa vitu mbalimbali kwa ajili ya kupambana na maambukizi ya virusi vya Corona kwa kijiji cha Malolo kilichoko wilaya ya Kilosa mkoani Morogoro.

 Akizungumza kabla ya kukabidhi msaada huo uliotolewa na taasisi ya Ghoada Asseta anayomiliki, Armi alisema kuwa jamii za wafugaji na wakulima wamekuwa wakipata changamoto kutokana na mwingiliano wa ardhi hivyo upendo na ushirikiano ndio njia pekee ya kuepuka migogoro hiyo nchini.

Alisema kuwa msaada huo una lengo la kuwakutanisha pamoja jamii hizo hasa katika kipindi hiki cha pambano dhidi ya kuenea kwa virusi vya corona ambalo ni janga la dunia hali iliyomlazimu kutumia misaada hiyo kudumisha upendo na ushirikiano miongoni mwao.

Alisema kuwa corona ipo na imegusa dunia nzima na hivyo masuala ya maendeleo lazima yaendelee kwa watu kufanya kazi kama ambavyo Rais Magufuli anasisitiza watu kufanya kazi hivyo lazima kujenga uhusiano mzuri katika jamii inayotuzunguka.

Armi alisema kuwa hali ya migogoro miongoni wa jamii za ufugaji na wakulima ikiendelea maendeleo hayatakuwepo zaidi kutakuwa na mapambano ambayo hayana faida kwa jamii na kudumaza maendeleo ya nchi.

Aliongeza kuwa katika kuwafanya jamii ya Malolo kufanya kazi kwa ushirikiano huku wakipambana na kuenea kwa virusi vya corona  ameamua kutoa msaada wa vitakasa mikono , mashine za kisasa za kutoa maji yanayotiririka kwa ajili ya shule za kijiji hicho, ndoo, vazi maalum kwa ajili ya wauguzi, mashine ya kupimia joto la binadamu na na barakoa vyote vikiwa na thamani y ash. Milioni 6.5

Akipokea vifaa hivyo afisa  mtendaji wa kata ya Malolo, Ferdinand Weteka kwa niaba ya mkuu wa wilaya ya Kilosa, alisema kuwa kwa msaada huo ambao umetolewa  na Brighton Armi  vifaa kinga hivyo vitawajengea ujasiri watoa huduma za afya katika kijiji hicho na kuwasaidia wanafunzi kuweza kujinga zaidi dhidi ya pambano ya kuenea kwa virusi vya Corona.

Alisema kuwa katika kijiji hicho hakuna kesi yoyote wala tetesi za kuwepo kwa mgonjwa wa virusi vya corona hivyo msaada huo umekuja katika wakati mwafaka na kumshukuru kwa niaba ya wananchi wa kijiji hicho na kutoa wito kwa wadau wengine kuangaza macho yao kwa wananchi wanaoishi vijijini.

Naye Afisa Elimu kata ya Malolo, Rehema Mwinuka alisema wamekuwa wakitekeleza afua mbalimbali za kuhakikisha wanafunzi waliofungua shule  wanakuwa salama dhidi ya ugonjwa wa COVID 19  kwa kutoa elimu ya namna ya kujikinga, huku akiongeza kuwa kijiji cha Malolo kipo vizuri na wananchi wengi wanaelimu ya pambano dhidi ya kuenea kwake.

Amemshukuru Armi  kwa kuwa msaada mkubwa kwenye shughuli za maendeleo katika kijiji hicho na kuwa mfano bora kwa jamii aliyokulia na kuzaliwa kwani ameonyesha njia na faida ya elimu kwa vijana wengi kutoka kijijini hapo.

No comments:

Post a Comment

Pages