HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

June 05, 2020

WANANCHI 319 WA KIJIJI CHA KIPANGEGE WILAYANI KIBAHA WAONDOKANA NA KERO SUGU YA MAJI

  Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Juma Aweso, akipiga makofi mara baada ya kumtwika ndoo ya maji kichwani Mbunge wa Kibaha Vijijini, Hamoud Jumaa, baada ya kukamilika kwa mradi wa maji katika kijiji cha Kipangege kilichopo kata ya Soga Wilayani Kibaha ambao tayari umeshaanza kutoa huduma ya maji safi na salama (Picha  Victor Masangu).
Mbunge wa Kibaha vijijini Hamoud Juma kushoto akitoa maelezo mafupi kwa Naibu Waziri wa Maji na Umwagiiaji kuhusiana na mwenendo mzima wa mradi huo wa maji katika kijiji cha Kipangege kilichopo kata ya Soga.

 
Victor Masangu, KIBAHA

WANANCHI wapatao 319 kutoka kijiji cha Kipangege kilichopo kata ya Soga Wilaya ya Kibaha Mkoa wa Pwani ambao walikuwa  wanasumbuka usiku na mchana kwa ajili ya kutafuta maji safi na salama hatimaye wameondokana na changamoto hiyo baada ya  kukamilika kwa mradi wa maji ambao umegharimu kiasi cha zaidi ya shilingi milioni 150.

Hayo yamebainishwa na Naibu Waziri wa maji na umwagiliaji Juma Aweso wakati wa ziara yak eta kikazi katika Wilaya ya Kibaha  Mkoa wa Pwani kwa ajili ya kukagua miradi mbali mbali ya maji na kutoa muda wa siku saba kwa uongozi wa Wakala wa  usambazaji wa maji na usafi wa mazingira vijijini Mkoa wa Pwani (RUWASA) kuhakikisha wanatekeleza maagizo yake aliyoyatoa  ikiwemo na ufungaji wa tanki kubwa la maji na kukemea vitendo vya ubadhilifu katika mradi huo.

“Nilikuja hapa mara ya kwanza kwa ajili ya kujionea mradi huu na niliambiwa kuwa ulikuwa na chanagamoto mbali mbali lakini  kwa leo hii imeamua kuja kuangalia utekelezaji wa maagizo ambayo niliyatoa juu ya upatikanaji wa maji kwa wananchi hawa,  lakini sambamba na hilo nimejionea maji yakitoka ili naagiza kwa mamlaza zinazohusika kufunga tanki la maji ili kuondokana  na changamoto ya maji kutoka kwa mgao,”Alisema Aweso.
Aweso alibainisha kwamba lengo kubwa la serikali ya awamu ya tono ni kuhakikisha kwamba inasimamia na kutekeleza kwa wakati  miradi mbali mbali ya maji ili kuweza kuwaondolea kero wananchi ambao wakati mwingine wamekuwa wakisumbuka kwa kutembea  umbari mrefu kwenda katika maeneo mengine kutafuta huduma ya maji.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa kijiji cha Kipangege  alisema  kwamba licha ya mradi  kukamilika  lakini bado kuna kero kubwa  kwa wananchi  kupata maji kwa mgao hivyo wameziomba mamlaka zinazohusika kulivalia njuga suala, huku Mbunge wa Jimbo la  Kibaha Vijijini Hamoud Jumaa akipongeza juhudi zilizofanywa na watendaji wa Dawasa na Ruwasa katika suala la upatikanaji wa  maji safi na salama kwa wananchi.

Naye Kaimu Meneja wa RUWASA Mkoa wa Pwani Injinia  Beatrice Kasimbazi amekiri na kusema kwamba mradi ho ulianza utekelezaji   kwa kipindi kirefu  tangu mwaka 2014 ambapo umeweza kukamilika mwaka huu kutokana na ushirikiano ambao wameufanya baina  yao pamoja na Dawasa kwa kuzirekebisha kasoro zilizokuwepo ikiwemo changamoto ya pampu pamoja na chanzo za maji.

"Huu mradi wa kikiji cha Kipangege kama nilivyoeleza hapo awaliulianza kufanyika tangu mnamo mwaka 2014 lakini kutokana na  kuwepo kwa changamoto mbali mbali kutoka kwa mkandarasi ambaye alipewa dhamani ya kuutekeleza alikuwa anamapungufu ndipo  tukaamua kushirikiana bega kwa bega na wenzetu wa Dawasa katika kukabiliana na kasoro ambazo zilikuwa zimejitokeza katika  kipindi cha nyuma na hatimaye kuweza kuzitafutia ufumbuzi,"alsiema Baatrice.

KUKAMILIKA kwa mradi wa maji katika kijiji cha Kipangege Wilayani Kibaha  ni moja ya hatua kubwa ya kuunga mkono juhudi za  Rais wa awamu ya tano Dr John Pombe Magufuli ambayo itakuwa ni mkombozi katika kumtua mama ndoo  kichwani sambamba na  kuwaondolewa wananchi hao adha kubwa ya  kutafuta maji usiku na mchana.

No comments:

Post a Comment

Pages