HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

June 01, 2020

Wateja HALOPESA kuzoa Bilioni moja

NA FRANCIS DANDE
KAMPUNI ya mawasiliano ya simu za mkononi ya Halotel kupitia huduma zake za kifedha za HaloPesa imejipanga kutoa gawio kwa wateja wake.
Hatua hiyo ikiwa ni hatua ya kwanza kwa HaloPesa kutoa gawio kiasi cha shilingi Bilioni moja kwa wateja wake Zaidi ya Milioni 1.9 ambao ni pamoja na wateja binafsi, mawakala na washirika wake mbalimbali wanatumia huduma za HaloPesa.
Akizungumza na waandishi wa Habari Mkuu wa kitengo cha biashara cha HaloPesa,  Magesa Wandwi alisema “Wateja watapata sehemu ya gawio hilo linalotokana na faida iliyozalishwa kutoka katika akaunti za HalotePesa Trust zilizoko katika mabenki mbalimbali nchini kati ya Oktoba 2016 na Desemba 2018.
Wandwi alisema kuwa faida hiyo ni haki ya wateja na hivyo HaloPesa tunashauku na furaha kubwa ya kuwalipa wateja wetu gawio hilo kwa mujibu wa sheria , kanuni na miongozo mbalimbali toka Benki kuu ya Tanzania (BOT).
“Gawio hili ni la kwanza kwa wateja wetu na litatolewa ndani ya mwezi mmoja toka sasa, kiasi cha gawio ambacho mteja wa Halopesa atakipata anaweza kutumia atakavyo ikiwa ni pamoja na kutoa au kufanya miamala mbalimbali, alisema na kuongeza
“Tunapenda kuwasihi wateja wetu kuwa Halotel tunaendelea na kutoa huduma bora zenye gharama nafuu nchi nzima na waendelee kutumia huduma zetu za HaloPesa,” alisema Wandwi.
 Mkuu wa Kitengo cha Biashara cha HaloPesa, Magesa Wandwi, akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo Juni 1, 2020 kuhusu kuanza kutoa gawio kwa wateja wake.
Katika muendelezo wa kutoa huduma bora za kifedha nchini.

No comments:

Post a Comment

Pages