HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

June 10, 2020

YANGA MOLINGA KIMENUKA

Na Mwandishi Wetu

WAGOMBANAPO Ndugu shika jembe ukalime, unaweza kueleza hivyo mara baada ya klabu ya Yanga na Mshambuliaji wao wa kimataifa David Molinga kuonyeshana mabavu kikosi kikitua mjini Shinyanga kwa ajili ya mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara.

Kikosi cha Yanga kiliondoka jana alfajiri na kufanikiwa kutua Shinyanga salama kuwakabili Mwadui FC ukiwa ni mchezo wa kwanza kutoka kwenye janga la Virusi vya Corona, ambapo Ligi ilisimama tangu Machi 17 mwaka huu.

Kwa mujibu wa taarifa za klabu kupitia App yao zilieleza kuwa Molinga amegoma kusafiri na timu kwa sababu zake binafsi jambo amablo liliukera uongozi na kuamua kumuacha.

Baaada ya taarifa hizo kushika kasi Molinga aliibuka na kukanusha taarifa hizo kupitia ukurasa wake wa Instagram akieleza kuwa hajagoma bali hakujumuishwa kwenye kikosi kinachoenda kuikabili Mwaduo juni 13.

“Nataka nikanushe hii habari kwamba nimegoma kusafiri na timu kwanza nimewakumbushe kitu cha peke imenileta Tanzania ni mpira na kazi yangu ndio iyo sasa iko ivi tangu timu imeanza mazoezi sijawahi kukosa na nafata ‘program’ za mwalim vizuri lakin jana orodha ilitoka na mimi jina langu ajakwepo sasa.

“Itasemekana vipi mimi nimegoma kama ndio ivyo muulizeni kocha ndio alitajia orodha yake, imekuwa tabia kila mara kila kitu mimi tu ata kama sjafanya kitu kibaya utaskia tu molinga ‘this is too much’imezidi sasa.”aliandika Molinga.

Akizungumza na Habari Mseto, Ofisa Habari wa Yanga Hassan Bumbuli amesema Molinga amegoma kusafiri na timu kwa sababu zake binafsi sio kwamba hajajumuishwa kwenye kikosi.

“Suala la Molinga niliandika mwenyewe kwe App yetu kwa sababu kilichotokea chote nilikishuhudia kwa macho yangu sijahadithiwa, yaani nikwamba wachezaji waliitwa kambini yeye hakuja kwa sababu hakukuwa na ufuatiliaji tu kajua atakuja.

“Alipopigiwa simu na Meneja akasema sawa najiandaa mnipitie Shekilango, tumetoka tumefika Shekilango akapigiwa simu hapokei, Meneja akashuka kwenye gari akamfuata nyumbani kwake akamgongea akafungua mlango akamwambia bwana twende akasema siendi sijui siko jina langu sikulisikia jana akaanza kueleza sababu tofauti na aliyoaeleza mwanzo.

“Kwaiyo sababu zake ziwe za msimu zisiwe za msingi hata kama anazieleza kwenye vyombo vya habari ni kwamba amegoma."amesema Bumbuli

Sakata hilo limechukua nafasi kubwa katika vyombo vya habari kiasi cha kuanza kuibuliwa hoja nyingine ambazo zinaonyesha kuwa ndani ya Yanga yawezekana hakuko salama.

Yanga wanatarajiwa kukata utepe jumamosi hii katika Uwanja wa Kambarage mjini Shinyanga dhidi ya Mwadui huku wakihitaji matokeo chanya kurudisha Imani na ari ya mashabiki baada ya kutoka kupoteza mchezo wa kirafiki dhidi ya KMC FC walipolala kwa mabao 3-0. Uwanja wa uhuru jijini Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment

Pages