HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

June 30, 2020

Yanga vs Kagera ni kisasi leo

Kikosi cha Yanga.
 
 
Na Mwandishi Wetu
 
KISASI juu ya kisasi unaweza ukasema kwenye mchezo wa leo kati Mabingwa wa Kihistoria wa Ligi Kuu Bara (VPL), Yanga SC dhidi ya Kagera Sugar ‘Wana Nkurukumbi’ utakaopigwa saa 1 jioni, Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
 
Mchezo huo ni wa kusaka nafasi ya kucheza nusu fainali ya Kombe la Shirikisho la Azam (ASFC), ambapo kila mmoja anahitaji kushinda ili aweze kusonga mbele.
 
Yanga inahitaji kulipa kisasi leo, baada ya kuchapwa mabao 3-0 dhidi ya Kagera Sugar kwenye  mchezo wa ligi kuu bara msimu huu, ambapo Wana Wana Nkurukumbi walivunja mwiko wa kutowafunga wanajangwani kwa miaka 10.
 
Akizungumzia mchezo huo Meneja wa Yanga Abeid Mziba alisema, vijana wao wapo sawa lengo lao kubwa ni kuweza kunyakua kombe la ASFC msimu huu baada ya kulikosa taji la VPL.
 
“Hali ya vijana wote wapo katika hali nzuri, timu imekamilika kiakili na kiafya wote wapo vizuri lengo letu kubwa tumeukosa ubingwa wa ligi kuu mwaka huu akili yetu tumeiweka kwenye ASFC.
 
“Kagera ni timu yenye mwalimu na wachezaji wazuri na wachezaji wetu wapo katika hali nzuri, nia na madhumuni yetu kufika fainali na tuchukue kombe la ASFC na safari hiyo tunainza leo,” alisema Mziba ambaye pia ni mchezaji wa zamani wa Yanga.
 
Naye Kocha wa Kagera Sugar Mecky Mexime alisema wachezaji wao wapo vizuri japo mchezo utakuwa mgumu wamejipanga kuondoka na ushindi na kuweza kusonga mbele.
 
Mchezo mwingine utakaopigwa leo, Namungo FC  itawakaribisha Alliance FC ya Mwanza Uwanja wa Majaliwa Ruangwa mkoani Lindi.
 
KESHO
Mchezo wa kukatana shoka utawakutanisha wababe wa soka nchini Azam FC dhidi ya Simba SC utakaopigwa Saa 1 jioni, Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Nao Sahara All Stars itawaalika Ndanda FC ya Mtwara Uwanja wa Mkwakani jijini Tanga.

No comments:

Post a Comment

Pages