HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

January 20, 2021

Serikali yajipanga kuondaoa majitaka Jijini Dodoma

 NA HAMIDA RAMADHANI, DODOMA


SERIKALI ipo kwenye hatua za mwisho za kuhakikisha kunakuwepo na uondoshaji mkubwa wa maji taka katika jiji la Dodoma unaojumuisha ujenzi wa kilomita 250 za mabomba pamoja na mabwawa 16 yatakayojengwa katika eneo la Nzuguni.

Hayo yamesemwa  leo Jijini hapa na Naibu Waziri wa Maji Maryprisca Mahundi alipokuwa akifungua Baraza la Sita la wafanyakazi wa DUWASA ambapo amesema lengo ni kuifanya Dodoma kuwa na sura ya Makao Makuu ya nchi.

Amesema ili mradi huo ufanikiwe kwa malengo yaliyokusudiwa lazima wananchi wapatiwe elimu ya kutosha kwani ni wachache wanaofahamu kuwa wanaweza kuunganishiwa mfumo huo kutoka  kwenye makazi yao hadi kupeleka maji taka kwenye mabwawa.

"Duwasa inatakiwa kutatua kero kwani kero nyingine zimekuwa zikisababishwa na baadhi ya watu ambao wanashindwa kufanya kazi kwa ufanisi,".

Na kuongeza kusema" Baadhi ya wananchi wamekuwa wakilalamika kutokana na huduma wanazozipata hivyo kupitia baraza hili hakikisheni mnafanya kazi ya kuzitatua kero hizo ili wananchi wafurahie uwepo wa mtandao wa maji," amesema Waziri Maryprisca.

Amesema kuna kila sababu ya Duwasa kuendelea kuujenga mtandao wa maji kwa kuwafikishia wananchi huduma za maji kwani wanauhitaji huo .

"Wizara itaendelea kuiwezesha ili iweze kutoa huduma bora kwa Wananchi," Amesema Waziri huyo.


Kwa upande wake Mhandisi Aron Joseph Kaimu Mkurugenzi Mamlaka ya maji safi na Usafi wa Mazingira DUWASA amesema wao kama Mamlaka wataendelea kutoa huduma bora ya maji safi na Usafi wa Mazingira kwa wanchi wote wa Dodoma.

"Licha ya Dodoma kuongezeka kwa watu kutokana na kutambulishwa rasmi kuwa ni jiji ili kukabili tatizo la ukosefu wa maji kwa wananchi miradi ya muda mfupi na miradi ya muda mrefu ambapo katika mradi wa muda mfupi jumla ya visima 20 vimeanza kuchimbwa,".

Na kuongeza kusema "Mradi mkubwa katika Ziwa Victoria utakaopitia Mkoa wa Singida mpaka Mkoa wa Dodoma na kuwanufaisha wakazi wa mikoa hiyo," amesema Muhandisi Aron.

Naye Mwenyekiti wa Bodi Mamlaka ya Maji safi na Usafi wa Mazingira DUWASA Faustine Bee amesema wamejipanga  kupunguza malalamiko kwa wakazi wa Dodoma juu ya upatikanaji wa maji na Usafi wa Mazingira katika makazi yao.

Pia amesema wamejipanga kuhakikisha wanadhibiti upotevu wa maji kutoka asilimia 26 mpaka kufikia 10 au kumaliza kabisa tatizo hilo.

No comments:

Post a Comment

Pages