HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

February 04, 2021

Wajumbe wa Menejimenti ya Wizara ya Mawasiliano naTeknolojia ya Habari wapigwa msasa

 NA HAMIDA RAMADHANI, DODOMA


WATUMISHI wa Umma wametakiwa kubadilika na kuacha kufanya kazi kimazoea na badala  yake wametakiwa kuzingatia Miiko na maadili ya uongozi.

Hayo yamebainishwa leo jijini Dodoma na Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Dkt Faustine Ndugulile alipokuwa akifungua mafunzo ya uongozi kwa wajumbe wa Menejimenti ya Wizara hiyo jijini hapa na kusisitiza maadili ya uongozi katika Utumishi wa umma.

Waziri huyo amesema kuwa watumishi wa Umma wamejisahau katika utendaji kazi wa majukumu yao ya kila siku mahala pakazi, badala ya kuhudumia Umma na kujiona kama vile wanajihudumia wenyewe.

Amewataka katika mafunzo hayo kufahamu dhana ya misingi ya uongozi kwa kuzingatia Miiko na maadili ya uongozi, Sheria na taratibu za Utumishi wa Umma,uongozi wenyetija na wakutatua changamoto ili kufikia Malengo na kuwa na uwajibikaji wa pamoja.

"Mafunzo Haya yamekuja katika muda sahihi kabisa na ukizingatia Wizara hii ni mpya imeundwa Desemba, 5 2020, mtambuka ,ya kimkakati na inagusa nyanja zote za kiuchumi na kijamii basi Hanna budi mpate mafunzo ya uongozi wa kutoka  Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania,"amesema Dkt Ndugulile.

Na kuongeza kusema kuwa" Nimeelezwa kuwa mafunzo haya yanalenga kuwajenga na kuwaimarisha ili muweze kuongeza buena kimkakati," Amesema.

Kwa upande wake Mhandisi Kundi Mathew Naibu Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari amesema mafunzo hayo yanawapa muongozo namna ya kwenda kutekeleza Ilani ya chama cha Mapinduzi (CCM) .

Amesema pia mafunzo hayo yanakwenda kuwakumbusha na kuwarudisha watumishi wa Umma katika Wizara hiyo mpya na kuwarudisha katika misingi ya Utumishi bora na wahaki.

Naye Naibu Waziri Ofisi ya Rais Utumishi na utawala bora Deogratius Ndejembi amesema wamefungua jambo sahihi kuwaita wanachuo cha Utumishi Umma ili kuwapiga msasa watumishi wa Wizara mpya ya Mawasiliano naTeknolojia ya Habari.

Ndejembi amesema chuo cha Utumishi wa Umma kipo kisheria na sio kama vyuo vingine kama Chuo Kikuu cha UDOM, Mzumbe au Chuo cha Dar es Salamu UDSM.

"Chuo hiki ni tofauti na vyuo vingine vya elimu ya juu mtu yoyote aliyemaliza kusoma  vyuo vya elimu ya juu na ni mtumishi wa Umma ni lazima apatiwe mafunzo katika Chuo cha Utumishi wa Umma," amesema Ndejembi.

No comments:

Post a Comment

Pages