HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

February 18, 2021

WIZARA YA KILIMO YAFANYA MAZUNGUMZO NA WADAU KILIMO KUHUSU MRADI WA MIAKA MINNE WA EURO MILIONI 100 KATIKA KUKUZA SEKTA YA KILIMO NCHINI


 

 

NA HAMIDA RAMADHANI DODOMA

 

 SERIKALI   kupitia Wizara ya kilimo imefanya kikao  cha pamoja na wadau wa kilimo kuhusu mradi wa miaka mine wenye thamani ya Euro Milioni 100.

Hayo yamebainishwa leo jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Kilimo Hussein Bashe alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kumalizika kwa kikao hicho.

Naibu Waziri huyo Bashe amesema lengo la kikao kazi hicho na Wadau wa kilimo ni kuangalia maeneo gani uwekezaji wa fedha unahitajika zaidi .

Aidha, Bashe amesema sehemu kubwa ya fedha katika mradi huo wa miaka minne inaenda kwenye miundombinu ya barabara ambapo ni Euro Milioni 48 .

 "Nasisitiza kupunguza gharama za utawala na gharama za semina ili kuwekeza zaidi kwenye miundombinu," amesema Naibu Waziri Bashe

Kwa upande wake mratibu mradi wa MARKUP  Safari Fungo amesema wamejikita zaidi katika kusaidia taasisi za kilimo kutafuta masoko na kuvutia mitaji kutoka nje ili kuvutia wawekezaji.

Mradi huo   wa miaka mine unaofadhilia na umoja wa Ulaya unaratibiwa na Taasisi ya MARKUP,AGRICOM,SELFIER na SOLIDAT .

No comments:

Post a Comment

Pages