HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

July 30, 2021

BAKWATA YAWATAKA WATANZANIA KUMLILIA MUNGU JUU YA UVIKO 19

 

 

Katibu Baraza la Ulamaa Bakwata Taifa, Sheikh Hassan Chizenga.

 

Na Upendo Kombe, Dar es Salaam

 

Licha ya kuzinduliwa kwa  chanjo ya uviko 19 Julai 28 2021 ikiwa ni jitihada za kupambana na wimbi jipya  la tatu la virusi vya corona, Baraza Kuu  la Waislam Tanzania (BAKWATA), limesisitiza umuhimu wa kumuomba Mungu ili hatupilie mbali janga hili.

 

Akitoa tamko la Baraza la Ulamaa Bakwata Taifa mbele ya waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Katibu Baraza hilo, Sheikh Hassan Chizenga, amesema  kuwa waumini wanatakiwa kuzingatia kuhusu chanjo ya  uviko 19 kuwa ibada ni jambo la muhimu na lakuzingatiwa hivyo ni vyema ibada  zote husika kuendelea lakini kwa kuchukua tahadhari zilizotolewa na  wizara ya afya. 

 

Sheikh Chizenga alisema kuwa waumini wanapaswa kungapamoja na matumizi ya  vitakasa mikono na vikalio, maji tiririka  na sabuni ,kuvaa barakoa ,kukaa umbali wa mita moja  kati ya mtu na mtu wakati wa ibada na  vikao mbalimbali  ili kuzuia madhara ya wahumini kuambukizana ugonjwa huo kabla na baada ya ibada.

 

 

 

Jina chizenga amesema jambo la kuabudu ni la muhimu sababu ndio kiunganishi cha mwanadamu na Mungu hapa ulimwenguni pia amezungumzia uwepo wa chanjo ni fursa kwa waislam kuweza kusafiri  kwenda  Hijja ikiwa ni utaratibu uliopo  kila mwaka.

Amesisitiza kuwa watu ambao wamethibitika kuugua  maradhi kama kisukari,pumu,presha na kansa kutokuhudhuria ibada na mikusanyiko mbalimbali ili kujiepusha na maambukizi yanayoweza kutokea  badala yake kufanyia swala na dua zao majumbani  na haitokuwa vibaya kufanya hivyo maana  swawabu za mtu huyo ziko pale pale   pia kutokana  na ufinyu wa nyumba  za ibada  baraza[U1]  linaomba ruksa ya kutumia barabara na sehemu za wazi kufanyia ibada hizo hata barabarani karibia na misikiti  husika.

 

 

Amesema ‘’ maandiko yanasema kuwa hakuna sababu ya mtu yeyote kujidhuru au kuwadhuru wengine kukwepa mikusanyiko kama wataalamu wa afya wanavyoeleza ili kulinda afya zetu pia Tanzania ni nchi ambayo Mungu amekuwa akiiepusha na majanga mbalimbali kama kipunga na mengineyo  hivyo tuendelee kumuomba Mungu maana ndio silaha yetu’’ Alisema.

 

Aliongeza kwakuipongeza serikali ya awamu ya sita kupitia rais Samia suluhu Kwakupokea na kuzindua chanjo ya johnson johnson ambayo niya hiyari kwa yeyote mwenye uhitaji  kufika  kuchanja katika vituo vya afya vyote nchini.

No comments:

Post a Comment

Pages