HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

July 30, 2021

NDAISABA KUMALIZA KIU YA WANANCHI ATATUA KERO MITA YA MITA ZA UMEME

 Na Lydia Lugakila, Ngara Kagera

 

Mbunge wa Ngara Ndaisaba Ruhoro  amefanya ziara wilayani Ngara na kukutana na wadau mbali mbali wakiwemo wa Kijiwe cha Kahawa kwenye Mji wa Kabanga pamoja na kuzungumza na wananchi zaidi ya 50 ambao walipata wasaa wa kupata mrejesho wa utekelezaji wa ahadi zake Wakati wa Kampeni za Uchaguzi mkuu ambapo kiu ya wengi ilikuwa ni kupata huduma ya mita za umeme kutokana na kufuata huduma hiyo Bukoba badala ya kuzipata wilayani humo.

 Wananchi hao waliopata nafasi ya kuuliza maswali ya aina mbali mbali  baadhi yalipata majibu na mengine yalichukuliwa kwa ajili ya utekelezaji.

Aidha baadhi ya maswali yaliyoulizwa na wananchi hao  ni pamoja na kutaka kujua ni  sababu zipi zinazofanya Mita za umeme kutouzwa wilayani  Ngara na baadala yake zinauzwa Bukoba hali inayoleta usumbufu kwa wananchi wanaohitaji mita hizo.

Miongoni mwa wauliza maswali ni pamoja  na mzee Said Manywele, huku mbunge wa jimbo hilo Ndaisaba Ruhoro  akiahidi kumaliza changamoto hiyo.

Baada ya hatua hiyo mbunge huyo, amefanya mawasiliano na Kaimu mkurugenzi mkuu wa TANESCO na baada ya mawasiliano hayo, TANESCO imeahidi kutoa maelekezo mkoani ili mita zifikishwe Ngara haraka ili wananchi waanze kupata  huduma kutokea Ngara.

 RUHORO ameishukuru TANESCO kwa utendaji wa kazi mzuri uliotukuka na kwa kuwa Tayari kujibu kero mbali mbali za wananchi ikiwa ni pamoja na kuzifanyia kazi.

No comments:

Post a Comment

Pages