HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

July 30, 2021

RC Makalla awaondoa hofu Watanzania Chanjo ya COVID-19 awashauri kuchanja kwa hiari

Hussein Ndubikile, Dar es Salaam


Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Amos Makalla amewaondoa hofu na kuwahakikishia Watanzania  Chanjo ya Ugonjwa Covid-19 ni salama huku akibainisha kuipokea kwa hiari ili kujikinga na wimbi la tatu la ugonjwa huo.

Ameyasema hayo jijini humo katika kikao kazi kilichomkutanisha na watendaji wa afya wa Jiji hilo, Wakuu wa wilaya, Wakurugenzi wa manispaa zote, Makatibu tawala na watendaji wengine wa lishe kilichojadili mikakati ya kujikinga na ugonjwa huo pamoja na lishe kwa Jamii.

Amesema wananchi wa Dar es Salaam na watanzania wanatakiwa kuondoa hofu kuhusu chanjo hiyo kwani tangu wako wadogo hakuna chanjo waliyochanjwa iliyotengenezwa nchini hivyo wanatakiwa kuipokea kwa hiari kuchanjwa lengo likiwa kukabiliana na janga hilo.

" Niwatoe hofu Watanzania tumepatiwa  tuipokee kwa hiari katika chanjo zote tulizopewa hajitengenezwa hapa ondoeni hofu chanjo hii iko salama tuchanje kwa hiari tujikinge na Corona  binafsi najisikia vizuri baada ya kuchanjwa," amesema Makalla. 

Amempongeza Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Dorothy Gwajima kwa kuendelea kukabiliana na ugonjwa kwa kutoa miongozo mbalimbali ya kujikinga pamoja na kutoa maelekezo kwa watendaji wa Serikali na mamlaka husika kuchukua hatua.

RC Makalla amempongeza Rais Samia Suluhu Hassan kwa umauzi wake wa kukubali kuingizwa chanjo nchini kwa ajili ya kujikinga na Corona pamoja na kuonyesha mfano wa kuchanjwa chanjo ya ugonjwa huo kwa hiari huku akisisitiza kufanya hivyo ni kukubaliana na ukweli wa dunia kuhusu ugonjwa huo.

Ameiagiza kamati ya ulinzi na usalama za mkoa kusimamia kanuni na miongozo ya kujikinga na ugonjwa huo ikiwemo daladala kutosimamisha abiria na watakopanda kuvaa barakoa pamoja na Kivuko cha Kigamboni kuzingatia kanuni hizo.

RC Makalla amewaagiza wakuu wa wilaya kuendelea kusimamia kanuni, shera na miongozo ya kupambana na Covid 19 pamoja na kutenga fedha za kutoa elimu na mafunzo kwa maafisa lishe ili kuwaongezea ujuzi katika shughuli zao.

Kwa upande wake Waziri Gwajima ameupongeza mkoa huo kwa hatua mbalimbali unaozichukua katika kukabiliana na ugonjwa huo na kusisitiza chanjo hizo zisichukue  siku 10 kuwafikia wananchi na kwamba maeneo yatakayolegalega kuzitoa watazichukua.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni kwa niaba ya wakuu wa wilaya waliopo Dar es Salaam ametoa shukrani kwa mkoa kwa kuandaa kikao hicho chenye lengo la kujikinga na ugonjwa huo nchini.

No comments:

Post a Comment

Pages