HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

November 17, 2021

TPSF yapokea msaada wa dola Milioni 700 kwa ajili ya Mradi wa Kukuza na Kuendeleza Wafanyabiashara wadogo kukuza chapa zao


Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF), Francis Nanai akizungumza leo jijini Dar es Salaam katika Uzinduzi wa Mradi wa kukuza Chapa za wafanyabiashara wadogo kuwa kubwa na kuziuza duniani.
Mkurugenzi Mtendaji wa TWCC Mwajuma Hamza akizungumza kuhusiana na wanawake wafanyabiashara kuchangamki fursa za Mradi wa AfRAP katika uzinduzi wake jijini Dar es Salaam leo.
 

 
Hussein Ndubikile, Dar es Salaam
 

TAASISI ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF) imepata msaada wa zaidi ya dola Milioni 700 kwa ajili ya Mradi wa Kukuza na kuendeleza wafanyabiashara wadogo kukua na chapa zao na kuuza duniani kote.

Msaada huo ni kutoka Benki ya Maendeleo Afrika (AfDB) ambapo Tanzania kwa nchi za Afrika Mashariki ndio ya kwanza kuwa na Mradi huo unaojulikana kama Africa Franchising Accelerator (AFRAP) 2021-2025.

Hayo yamesemwa leo jijini Dar es Salaam katika Uzinduzi wa mradi huo na Mkurugenzi Mtendaji wa TPSF, Francis Nanai ambapo amesema mradi utazalisha ajira za moja kwa moja 38,000 na zile zisizo moja kwa moja ni ajira 56,000.

Amebainisha kuwa  wafanyabiashara wa wakikuza chapa na kuuza duniani kote watasaidia katika ukuaji wa uchumi na kufanya nchi kuwa imara kiuchumi.

Mkurugenzi huyo amesema kuwa baadhi ya kampuni ambazo zilianza ukuaji huo ni Pepsi, Coca Cola, KFC ambazo Chapa zake zilikuwa zinauzwa na kueneaa Duniani hali ambayo wafanyabiashara wadogo wanaanza kujengwa kufika huko.

Amesisitiza kuwa Rais Samia Suluhu Hassan amefungua Uchumi wa Nchi hivyo ni kazi ya watanzania kuchangamkia fursa hiyo ambapo TPSF ipo kwa ajili ya kuona biashara zinakua kwa kasi.

Nanai ameongeza kuwa vigezo vya kuingia kwa wafanyabiashara wadogo kwanza ni kuwa na leseni za biashara ,kampuni zao ziwe zimekaguliwa mahesabu kwa miaka mitatu mfululizo,Mauzo ya Biashara kwa mwaka sh.milioni 250 pamoja na ulipaji kodi katika mifumo iliyowekwa na nchi.

Amefafanua kuwa mradi utachukua miezi 48 ambapo wataanza na mafunzo visiwani Zanzibar kuanzia Novemba 22 mwaka huu na kwenda Jijini Mwanza ,Mbeya na mikoa mingine huku Dar es Salaam itapata mafunzo mwakani.

"Mradi huu haufanywi kihuni huni ndio maana vigezo hivyo ni kwa ajili ya kupata washindani ambao wana uwezo wa kukuza chapa zao na Taifa  kuwa na wafanyabiashara wenye chapa zao kuzunguka ulimwenguni,"amesema Nanai.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha Wafanyabiashara Wanawake Tanzania (TWCC) Mwajuma Hamza amesema kuwa wanategemea wanawake asilimia 50 wataingia katika mradi huo na kuinuka na chapa zao.

Nae, Mshauri wa Mradi wa AFRAP Wambugu wa Gichohi amesema kuwa mradi huo umekuja kuinua biashara kwa kukuza chapa 'Brand' na kuingia katika ushindani wa masoko nje Tanzania.

 

No comments:

Post a Comment

Pages