Hussein Ndubikile, Dar es Salaam
Filamu
ya Binti (2021) yazidi kuipeperusha bendera ya Tanzania duniani tayri
filamu hiyo imeshafanya vizuri kwenye matamasha mbalimbali yakiwemo Pan
Afican Film Festival ya Los Angeles, USA, Durban Film Festival ya South
Africa pamoja na matamasha nchini Nigeria.
FIlamu
ya Binti imeshinda tuzo ya filamu bora ya mwaka 2021 kwenye tamasha la
Filamu la ZIFF-Zanibar na sasa itaonekana kwenye jukwaa la Netflix
duniani kote ambapo jukwaa hilo lona watazamaji zaidi ya 200,000,000.
Akizungumza
jijini Dar es Salaam na Wanahabari, Mwandishi na Muongozaji wa Filamu
hiyo, Seko Shamte amesema Filamu yake tayari imeshaanza kuonekana katika
jukwaa la Netflix kuanzia Tarehe 07 Januari, 2022.
“tumepata
nafasi ya kuoneshwa Duniani kote, kuna kazi zingine kutoka Afrika
hazionekani nje ya Afrika, lakini Filamu yetu imepata bahati ya
kuonekana kila pembe ya Dunia bila kikwazo chochote” alisema Bi. Seko
Shamte.
Amebainisha,
Filamu hiyo imetayarishwa na Wanawake, kuanzia Uandishi wa mswada,
Uigizaji, Uongozaji na Uhariri, hivyo mafanikio ya kazi hiyo ni ishara
ya ukuaji wa uwezo wa Wanatasnia Wakike nchini.
Ameishukuru
Serikali kwa kumuunga mkono katika mafanikio ya filamu yake tangu hatua
ya Utayarishaji hadi sasa kuonekana Netflix. Aidha, alimalizia kwa
kutanabaisha kuwa, mafanikio ya Filamu hiyo yanaenda sambamba na
kuitangaza Nchi Kimataifa.
Katibu
Mtendaji wa Bodi ya Filamu Tanzania Dkt. Kiagho Kilonzo amewapongeza
Watayarishaji kwa hatua hiyo kwakuwa ni kwa mara ya kwanza Filamu kutoka
Tanzania kuoneshwa katika jukwaa hilo, ambapo ni nchi Tatu pekee kutoka
Afrika zimeshapeleka Filamu zao, ambazo ni Kenya, Nigeria na Afrika
Kusini, ila kwasababu ya ubora, Filamu yetu imefanikiwa kwenda huko.
Dkt.
Kilonzo ameeleza kuwa, mafanikio hayo ni mapinduzi kwenye Tasnia ya
Filamu nchini, kwani imepiga hatua kubwa katika eneo la Usambazaji,
ambapo sasa inasambazwa kupitia jukwaa kubwa linalotazamwa na Watazamaji
zaidi ya milioni 200 Duniani.
Kwa
upande wake Rais wa Shirikisho la Filamu Tanzania (TAFF) Eliya Mjatta
ametoa rai kwa Wadau wa Filamu na Watanzania kwa ujumla kuiunga mkono
filamu hiyo kwa kuitazama katika Jukwaa la Netflix ili kuonesha tija ya
kazi hiyo katika Mtandao huo.
Naye
Mshindi wa Tuzo ya Muigizaji Bora kupitia Tuzo za Filamu Tanzania 2021,
Godliver Gordian amewasahauri Watayarishaji kutayarisha Filamu zenye
uhalisia wa Maisha ya Jamii zetu kama ilivyo Filamu ya Binti, na ndio
maana imefanikiwa kufika mbali.
Filamu
hiyo imefanikiwa kuoneshwa kwenye matamasha makubwa ya Filamu katika
nchi za Marekani, Ujerumani, Nigeria, Afrika Kusini na New Zeland.




No comments:
Post a Comment