Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum yatambulishwa rasmi
Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Dk. Dorothy Gwajima akizungumza na Menejimenti ya Wizara yake.
NaAsha Mwakyonde, Dodoma
WAZIRI wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Dk. Dorothy Gwajima amesema kuwa Wizara hiyo ipo tayari kutekeleza majukumu yake sambamba na maagizo mbalimbali ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan katika kufikia azma yake ya kuwaletea wananchi Maendeleo.
Dk.Gwajima ameitambulisha rasmi jana wizara hiyo kwa Umma na kuwahakikishia kuwa itafanyaka kuwa mwanga katika kuongeza kasi kwenye Maendeleo ya Jamii.
Waziri Dk.Gwajima ameyasema hayo jana Jijini Dodoma kwenye Ofisi za Wizara zilizoko Mji wa Serikali, Mtumba wakati akizungumza na Menejimenti ya Wizara hiyo katika kikao cha kwanza kukutana tangu kuanzishwa kwa Wizara hiyo Mpya.
"Rais Samia Suluhu Hassan ameona umuhimu wa kuwepo kwa Wizara Ili iweze kuratibu na kuhakikisha wananchi wa makundi yote wanashiriki kusukuma maendeleo ya Taifa lao Sekta zote" alisema Dk.Gwajima.
Waziri Dkt. Gwajima ameongeza kuwa Wizara yake itashirikiana na wananchi na wadau wote katika kuhakikisha kuwa inakuwa kiungo katika kuhakikisha Jamii inakuwa na maendeleo na Ustawi.
Hatua hii inakuja mara baada ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan kuanzisha Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum yenye lengo la kuhakikisha jamii inapata Maendeleo na Ustawi wao.




No comments:
Post a Comment