HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

February 20, 2022

Benki ya CRDB yatoa elimu ya fedha kwa Machinga DAR

 

Meneja wa Benki ya CRDB Kanda ya Mashariki, Badru Idd akizungumza wakati wa ufunguzi wa Semina ya Elimu ya Fedha kwa  Shirikisho la Umoja wa Wamachinga mkoa wa Dar es  Salaam lililoendeshwa na Benki ya CRDB leo Februari 20, 2022 jijini Dar es Salaam. 
Mkuu wa Kitengo cha wateja binafsi Benki ya CRDB, Stephen Adili akizungumza wakati wa ufunguzi wa Semina ya Elimu ya Fedha kwa Machinga iliyoendeshwa na Benki ya CRDB leo Februari 20, 2022 jijini Dar es Salaam. Mafunzo haya yamehudhuriwa na  Shirikisho la Umoja wa Machinga Mkoa wa Dar es  Salaam (Machinga Saccos) na baadhi ya wawakilishi wa wafanyabiashara hao kutoka  mikoa yote Tanzania ikiwa ni mwendelezo wa ushirikiano  kati ya Benki ya CRDB na wafanyabiashara wadogo.
Makamu Mwenyekiti wa Shirikisho la Umoja wa Wamachinga mkoa wa Dar es  salaam, Steven Lusinde akizungumza wakati wa ufunguzi wa Semina ya Elimu ya Fedha kwa Shirikisho la Wamachinga Mkoa wa Dar es Salaam lililoendeshwa na Benki ya CRDB leo Februari 20, 2022 katika ukumbi wa PTA Sabasaba, Dar es salaam.

No comments:

Post a Comment

Pages