NA TATU MOHAMED
KAMISHNA
wa Mamlaka ya Usimamizi wa Shughuli za Bima Nchini (TIRA) Dk. Baghayo
Saqware amesema serikali ipo tayari kushirikiana na Shirika la bima la
Taifa (NIC) kwa kuhakikisha inawafikia wakulima, wafugaji, na wavuvi
wote nchini.
Dk. Saqware
ameyasema hayo jana alipotembelea katika banda la NIC lililopo katika
Maonesho ya 46 ya Biashara ya kimataifa (DITF) yanayoendelea katika
viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere Jijini Dar es salaam.
Amesema
serikali imekuwa ikitegemea sana Shirika la NIC katika kuendeleza soko
katika maeneo ya bima ya kilimo, majengo, pamoja na bima mbalimbali.
Dkt
Sqware amesema NIC ni wazoefu zaidi katika soko la bima kutokana na wao
kuwa na mtaji mkubwa na wataalamu wa kutosha katika soko.
“Ukizungumzia
bima Tanzania hakuna namna unaweza kuisahau NIC kwa maana ya wataalamu,
uzoefu pamoja na mtaji,” amesema Dk. Saqware.
Vilevile
amesema hivi karibuni NIC wamejikita katika bima ya kilimo ambapo
amewapongeza kwa hatua hiyo na kuhaidi kuendelea kushirikiana nao.
“Tayari
tumewapatia namba viongozi wa NIC ili waweze kuwasiliana na viongozi
wa wakulima na wafugaji hapa nchini ili waaze kuangalia ni kwa namna
gani wanaweza kuwafikia zaidi na kuwapatia bima," amesisitiza.
Naye
Mkurungezi wa Masoko na huduma kwa wateja NIC, Yesaya Mwakifulele
amesema katika Maonesho hayo NIC imejikita katika ushiriki kikamilifu
kwa kuhakikisha inatoa huduma mbalimbali kuhusu suala nzima la bima.
Amesema
katika Maonesho hayo wamekuja na APP ya NIC kigajani ambayo
inamuwezesha mteja kupata huduma akiwa nyumbani bila ya kufika katika
ofisi zao.
“Kupitia APP
hiyo mteja anaweza kujihudumia kwa hatua chache tu ambayo ataweza kukata
bima ya aina mbalimbali ikiwemo nyumba, gari.
Akizungumzia
kuhusu suala nzima la madai amesema NIC imekuwa ikifanya ulipaji huo
ndani ya siku saba tu iwapo taarifa zote zikiwa sawa.
“Kwa sasa hatuna madai yoyote ambayo ayajalipwa labda yale ambayo taarifa zake aziko sawa,” amesema Mwakifulele.
Aidha
amewataka watanzania wote kwa ujumla kufika katika banda lao ili
waweze kupata elimu pamoja na huduma za uhakika za bima ambazo
zitaweza kumsaidia pale anapopata majanga.
No comments:
Post a Comment