HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

January 26, 2023

Mico Halal, Wafanyabiashara wakutana kujadiliana Idhibati za Bidhaa Kongamano la Biashara Halal

 Na Hussein Ndubikile, Dar es Salaam


Taasisi ya Kimataifa ya Ithibati (Viwango) Mico imefanya Kongamano la Kwanza lililowakutanisha wafanyabiashara jijini Dar es Salaam kwa lengo la kujadiliana na kutoa elimu na kuweka wazi masoko ya bidhaa mbalimbali ya Biashara Halal


Akizungumza katika kongamano hilo jijini Dar es Salaam Kaimu Mufti Mkuu wa Tanzania Skeikh Hamid Jongo ameipongeza taasisi ya Halal kwa kuandaa kongamano hilo.

Amesema kuwa uwepo wa taasisi hiyo nchini ni jambo jema kwani imekuwa ni kiu ya muda mrefu kwa wafanyabiashara na Serikali.

Skeikh Jongo amebainisha kuwa uwepo wa taasisi hii nchini itasaidia kutoa uthibati kwa bidhaa mbalimbali hivyo kusaidia kupenya katika masoko ya ndani na nje na kuchangia pato la Taifa.

“Tumekuwa tukikosa soko la kuuza bidhaa, hivyo wafanyabiashara bidhaa zao zitathibitishwa kupitia Halal na hivyo kuongeza mapato kwa kwa Serikali,” amesema Sheikh Jongo.

Ameongeza kuwa taasisi hiyo itasaidia kupatikana kwa bidhaa bora kama vile za chakula, nguo na kadhalika kwa ajili ya afya njema za wateja.

Amesisitiza kuwa Baraza la Waislamu Tanzania (BAKWATA) linaunga mkono na kupongeza  jambo hilo kwani litasaidia Mtanzania kula chakula safi, mavazi safi na hivyo kuwa na maisha mazuri.

Pia amesema kuwa wafanyabiashara wa Tanzania wamekuwa wakienda nchi zingine kwa ajili ya kufata ithibati ya bidhaa zao hivyo Halal itawarahisishia kupata ithibati ndani ya nchi.

“Kwa kupatikana kwa Taasisi ya Halal itasaidia na kuwezesha kuwa rahisi kwa wafanyabiashara kupata ithibati na kufanya biashara ndani na nje,” ameongeza Sheikh Jongo.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa TanTrade, Latifa Khamis amesema soko la Halal limekwenda kimataifa hivyo kupitia Halal wafanyabiashara watasaidiwa kujua bidhaa halali na zisizo halali ili kuweza kuhimili soko la ndani na nje.

“Kupitia taasisi hii wafanyabiashara hili waweze kufanya vizuri wanatakiwa kijua Halal ni nini, naomba waitumie sana Halal kwani itawapatia ithibati ya bidhaa zao,” amesema Latifa.

Mapema akiongea katika kongamano hilo Naibu Mkurugenzi wa Mico Halal, Muhamed Juma amesema kongamano hilo ambalo linafanyika kwa mara ya kwanza lengo lake ni kujadiliana, kubainisha, kuelimisha na kuweka wazi masoko.

Amefafanua kuwa kongamano hilo limewaleta pamoja wafanyabiashara na wasio wafanyabiashara kwa lengo la kujifunza na kupata ufahamu kuhusu Halal.

No comments:

Post a Comment

Pages