HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

February 24, 2023

Sheria mpya ya watu ulemavu yaleta matumaini kwa watoto wanaofichwa

  Yaharamisha kuwafungia watu wenye ulemavu

Dk. Martin Luther King Jr, akizungumzia safari ndefu ya kuanzisha usawa kati ya jamii zote, alisema ‘the arc of the moral universe is long, but it bends towards justice’. Kwa tafsri isiyp ramsi “taa ya ulimwengu wa maadili ni ndefu, lakini inainama kuelekea haki’.

Kauli hiyo imetumika kote ulimwenguni katika kusukuma mageuzi ya kijamii, ikibainika kuwa mabadiliko hayaji mara moja, lakini polepole.

Msukumo wa haki za watu wenye ulemavu Zanzibar ulianza miaka ya 90 wakati Umoja wa Watu Wenye Ulemavu Zanzibar (UWZ) chini ya hayati Mwalimu Khalfan, uliposhika bango la kutetea haki za watu wenye ulemavu na kushinikiza kuwa na serikali yenye masikio ya kusikia sauti zao.

Msukumo huo uliingiza hali ya kujitambua katika jamii ambayo kwa muda mrefu ilikuwa haijajali haki za watu wenye ulemavu.

Hata hivyo,  dhamiri hii mpya haikupuuzwa. Hatua kwa hatua, wadau  wengi zaidi, wakiwemo marais, jumuiya ya kimataifa na asasi za kiraia walichangia kikamilifu kusukuma mbele ajenda ya watu wenye ulemavu kutoka kupitishwa na kutumika Sheria ya Watu Wenye Ulemavu (Haki na Fursa) Namba 9 ya mwaka 2006 na hadi kutunga Sheria mpya ya 2022 ambayo Rais aliidhinisha terehe 22 Desemba, 2022.

Sheria mpya ya Watu Wenye Ulemavu ya 2022, inaleta maelfu ya manufaa, yote yakidhamiria kusawazisha kasoro, madhila na shida wanazopitia watu wenye ulemavu na kuweka fursa sawa kwa wote.

Kwa kutaja machache yaliyomo katika sheria hii mpya: Watu wenye ulemavu wana haki ya kupata elimu inayojumuisha mafunzo ya ufundi stadi na mafunzo ya kukabiliana na hali ya kijamii kwa kuzingatia aina ya ulemavu; haki ya kufanya kazi na ajira; haki ya kupata huduma za afya; haki ya kupata habari na mawasiliano, uanzishwaji wa Baraza la Taifa la Watu Wenye Ulemavu na uanzishwaji wa Mfuko wa Maendeleo ya Watu Wenye Ulemavu Zanzibar.

Hata hivyo, kazi zaidi inapaswa kufanywa. Serikali ilitenga Sh1.07bilioni kwa Baraza la Taifa la Watu Wenye Ulemavu lililoanzishwa chini ya sheria hiyo katika bajeti ya mwaka wa fedha 2022/2023, ambazo zinafadhili shughuli zinazolenga kuboresha ustawi wa kijamii na kiuchumi wa watu wenye ulemavu. Fedha hizo bado hazitoshi kuhudumia maelfu ya watu wenye ulemavu waliopo nchini.

Sheria mpya ya 2022 inaimarisha zaidi nafasi ya watu wenye ulemavu.

Chini ya kifungu cha 42 cha sheria hiyo, ni kosa kumficha mtu mwenye ulemavu.

Kifungu hicho kinasema: Mtu yeyote anayemficha mtu mwenye ulemavu anatenda kosa na akitiwa hatiani atatozwa faini isiyopungua shilingi elfu hamsini na isiyozidi shilingi laki tano.

Sheria hiyo pia inasema iwapo mtu mwenye ulemavu atatiwa hatiani kwa kosa lolote kwa mujibu wa sheria husika na kuhukumiwa kifungo chuo cha mafunzo, adhabu atakayopangiwa ilingane na hali na na aina ya ulemavu wake.

Kama sehemu ya jumuiya ya kimataifa, sheria mpya pia inaitaka serikali kuhakikisha na kuchukua hatua za kuzuia ulemavu unaosababishwa na ajali za barabarani, maradhi na mambo mengine ya kiafya; ajali, maradhi na majanga ya viwandani na mambo mengine yanayosababisha ulemavu.

Ahadi zilizotolewa na serikali katika sheria mpya ni kwa ajili ya uzalishaji wa data sahihi zilizogawanywa kulingana na aina za ulemavu, ahadi ambazo tayari ziko kwenye mkondo na uanzishaji wa mfumo mpya wa usajili.

Huku sheria ya watu wenye ulemavu ikiwa ya kwanza ambayo inajumuisha haki nyingi katika historia ya Zanzibar, bila shaka haikukusudiwa kuwa ya mwisho.

Hakika, sheria hii inaakisi ukweli kwamba sheria ya zamani ya 2006, haikuendana na mabadiliko ya nyakati. 

Wakati wa maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Watu Wenye Ulemavu Desemba mwaka jana, Makamu wa Kwanza wa Rais, Othman Massoud Othman, alisisitiza azma ya serikali ya kutunga sheria bora zitakazolinda haki za watu wenye ulemavu.

Pia katika shetia kuna kifungu cha haki ya kuishi kwa kujitegemea na kujumuishwa katika shughuli za kijamii, kiuchumi na kisiasa, pamoja na haki ya kushiriki na michezo na burudani.

Kama kwa sheria nyengine, sheria hii inaweza isikidhi matarajio na shauku yote waliyokuwa nayo wadau na watu wenye ulemavu, hata hivyo, ni nafuu ikilinganishwa na sheria iliyopita, na ni hatua moja  mbele katika kujumuisha na kupigania haki za watu wenye ulemavu Zanzibar, huku vizazi vijavyo vikitarajiwa kuendelea kuiboresha kama kilivyofanywa na kizazi cha sasa katika harakati za kutetea kundi hili.

Hata hivyo, wakati moja ya malengo ya sheria hii ni kuhakikisha ulinzi na fursa sawa kwa watu wenye ulemavu, maswali yanabaki juu ya utekelezaji wake.

Kama mwanga wa matumaini katika bara Afrika, sisi (Zanzibar) tujitahidi kila wakati kupiga ngumi kulingana na  uzito wetu na kupima kazi yetu dhidi ya bora zaidi ulimwenguni.

Sheria ya Wamarekani wenye Ulemavu inasalia kuwa sheria ya kihistoria kwa  watu wenye ulemavu. 

Bunge la 101 la Marekani lilipitisha sheria hiyo baada ya kupata uungwaji mkono mkubwa katika mgawanyiko wa kisiasa katika Bunge la Congress.

Mnamo Julai 26, 1990, Rais George H. W. Bush alitia saini sheria hiyo.

Ni matumaini ya watu wenye ulemavu wa Zanzibar kuwa sheria ya sasa italeta msukumo na kuongeza furaha waliyoikosa kwa muda mrefu.

No comments:

Post a Comment

Pages