HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

March 08, 2023

TANZIA: MWANDISHI WA HABARI AFARIKI KWA AJALI YA GARI

 


Klabu ya waandishi wa habari ya Mkoa wa Mwanza (MPC) inasikitika kutangaza kifo cha Mwanachama wake Richard Makore kilichotokea jana lwenye ajali ya gari (Min bus) iliyotokea Mkoani Geita.

Makore alikuwa anafanya kazi na Gazeti la Nipashe Mwanza na pia ni Mwanachama hai wa MPC.

Kwa sasa mwili wake upo kwenye chumba cha kuhifadhi Maiti hospitali ya Geita.

MPC inawaomba wanachama wake wote kuwa watulivu kwenye wakati huu mgumu kwetu.

Pia MPC inaendelea kuwajuza kila hatua ya inayoendelea.

Bwana alitoa na Bwana ametwaa jina lake lihidimiwe.

*Edwin Soko*
*Mwenyekiti*
*MPC*
*8.03.2023*

No comments:

Post a Comment

Pages