HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

May 05, 2023

HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA TANGA BOMBO KUNUNUA BASI


Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo Dkt Juma Ramadhani akizungumza wakati alipotembelea mabanda mbalimbali.

 

Na Oscar Assenga, TANGA 

KAIMU Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo Dkt Juma Ramadhani leo amewaongoza wauguzi katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa kwenye maaadhimisho ya siku ya Wauguzi Duniani ambapo kilele chake kitafanyika Mei 12 Jijini Mwanzasiku ya wauguzi Duniani. 

Maadhimisho hayo yalianza na maandamano kutoka eneo la Toyota mpaka Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo kulipofanyika kilele cha maadhimisho hayo

Akizungumza wakati wa maadhimisho hayo,Dkt Juma alisema kutokana na uwepo wa changamoto ya usafiri kwenye mkoa huo ambayo ilielezwa wakati wa risala ya wauguzi hao alieleza mipango ya uongozi wa hospitali hiyo kwenye bajeti zijazo na jitihada walizoweka kama taasisi wana mpango wa kununua basi. 

“Kwa sasa Hospitali kwenye bajeti zijazo na jitihada tulizowekeza taasisi wana mpango wa kununua basi kwa ajili ya hospitali  “Alisema Kaimu Mganga Mfawidhi Dkt Juma. 

Awali akisoma risala hiyo Katibu wa Tana Tawi Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Mwanaisha Nyangasa alisema maadhimisho hayo ni kutafakari na kufauta nyayo za mwanzilishi wa huduma za uuguzi na ukunga Bi Florence Night Ngare. 

Alisema wauguzi katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo wamemuenzi kwa kutoa huduma mbalimbali wakati wa maadhimisho hayo ikiwemo za uchunguzi wa saratani ya kizazi na matiti kwa wakina mama ,uchunguzi wa kisukari na macho,shinikizo la damu,kuhamasisha uchangia damu ,upimaji wa VVU kwa hiari na sambamba na utoaji elimu ya afya na lishe kwa wateja mbalimbali 

Aidha alisema pia katika maadhimisho hayo wametoa chanjo za Covid 19 ambapo wananchi waliohudumiwa tokea walipoanza maadhimisho hayo ni 154 ambao walihudumiwa kwa siku moja. 

Hata hivyo alisema kwamba Ukunga ni kada muhimu sana katika kufanikisha utoaji wa huduma nzuri za afya kwenye jamii na unapozungumzia afya bora muuguzi ni sehemu sahihi ya kufanikisha kila mtanzania anakuwa na afya bora. 

Alisema kwamba pamoja hayo kuna mafanikio makubwa ikiwemo mazingira ya kufanyia kazi yameboresha na miundombinu ya hospital na kuwezesha wanafanyakazi kufanya kazi kwenye mazingira mazuri. 

Aidha alisema kwamba pia ni wauguzi kupata nafasi ya kujiendeleza kimasomo,wauguzi kupata motisha mbalimbali,kuongezeka kwa hamasa kwa wauguzi . 

Akizungumzia changamoto wanazokabiliana nayo alisema kwamba changamoto kubwa ni upungufu wa watumishi idara ya ukunga na uuguzi kulingana na mahitaji ya jamii kutokana na kuongezeka kwa vitengo na idara ambazo wauguzi wanahitajika. 
 

No comments:

Post a Comment

Pages