HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

July 08, 2023

DC MATINYI APONGEZA JUHUDI ZA RAIS SAMIA SULUHU HASSAN KUWAWEZESHA VIJANA

 Mkuu wa  Wilaya ya Temeke, Mobhare Matinyi (kulia),  akizungumza  na  mjasiriamali kwenye banda  mojawapo  katika Maonesho ya 47 ya Biashara ya Kimataifa Julai 7, 2023  yanayoendelea kwenye viwanja vya SabaSaba  Barabara ya Kilwa, Dar es Salaam.

DC  Matinyi akiwa katika picha ya kumbukumbu na baadhi ya wafanyakazi wa Manisaa ya Temeke kwenye banda  lao  katika maonesho hayo.

Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Mobhare Matinyi  akiwa katika  picha ya kumbukumbu na baadhi  ya wanufaika  wa mikopo  ya asilimia  10 iliyotolewa na Rais Dk. Samia Suluhu Hassan.
 

Na Khadija Kalili

MKUU wa Wilaya ya Temeke,  Mobhare Matinyi, amepongeza ubora wa bidhaa za wajasiriamali waliowezeshwa kwa mikopo ya asilimia  kumi  na kuwataka waongeze uzalishaji ili wauze katika soko la kimataifa.

 DC Matinyi amewashauri  wajasiriamali waliowezeshwa kwa kupata mikopo ya asilimia kumi inayotolewa na Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan, kuboresha  bidhaa  zao ili ziweze kuleta  ushindani kwenye Soko la Kimataifa.

DC Matinyi amsema hayo leo Julai 7 2023 wakati alipotembelea mabanda  ya wajasiriamali hao katika Maonesho ya Biashara Kimataifa yanayoendelea katika viwanja  vya SabaSaba Dar es Salaam.

"Nimefurahi kuona wajasiriamali wakitumia fursa ya mikopo iliyotolewa na Rais wetu, Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika juhudi za kupambana na tatizo la ajira lakini changamoto yetu kubwa siyo kwa Temeke tu bali nchi nzima ni namna ya kulipata soko la kimataifa. Tupambane hadi tufikie soko la Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) na lile la Afrika nzima kupitia Mkataba wa Eneo Huru la Biashara Barani Afrika, amesema Matinyi.

Akijibu swali kuhusu tatizo la wananchi kuvamia maeneo ya wazi yanayomilikiwa na serikali, Mkuu wa Wilaya huyo ametoa  wito kwa Idara ya Ardhi kuwaelimisha wananchi mara kwa mara na hata kuweka matangazo ili maeneo hayo yajulikane na kuepuka watu kuyavamia.

No comments:

Post a Comment

Pages