HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

July 07, 2023

NAIBU KATIBU MKUU WIZARA YA FEDHA ATEMBELEA BANDA LA UTT AMIS KWENYE MAONYESHO YA SABASABA 2023

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Jenifa Omolo (kushoto), akisaini kitabu cha wageni alipotembelea Banda la Kampuni ya Uwekezaji ya UTT AMIS kwenye Maonesho ya 47 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba) Barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam. Katikati ni Afisa Mkuu wa Masoko na Uhusiano wa Kampuni ya Uwekezaji ya UTT AMIS, Martha Mashiku, Afisa Masoko na Mahusiano Mwandamizi wa UTT AMIS,  Grace Ngailo (kulia) na tatu kulia ni Afisa Masoko UTT AMIS, Waziri Ramadhani.
Baadhi ya wananchi waliotembelea Banda la UTT AMIS wakipata maelezo kuhusu Akiba na Uwekezaji kupitia mifuko ya Uwekezaji wa Pamoja inayoendeshwa na UTT AMIS wakati wa Maonesho ya 47 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba) yanayoendelea jijini Dar es Salaam.

 

Afisa Mkuu wa Masoko na Uhusiano wa Kampuni ya Uwekezaji ya UTT AMIS, Martha Mashiku (katikati), akiwa katika picha ya pamoja na watumishi wa kampuni hiyo. Kutoka kushoto ni Afisa Masoko Mwandamizi, Rahim Mwanga, Afisa Masoko, Doris Mlenga, Afisa Masoko na Mahusiano Mwandamizi, Grace Ngailo na Afisa Masoko, Waziri Ramadhani.

No comments:

Post a Comment

Pages