JESHI
la Polisi Mkoa wa Songwe limewaonya askari wenye ndoa wanapozaa watoto
kuacha tabia ya kuwapeleka kwa bibi na babu wakalelewe huko, kwa kuwa
kufanya hivyo husababisha malalamiko, huku wengi wao kukosa huduma
muhimu na uangalizi wa karibu zaidi.
Angalizo
hilo lilitolewa mwishoni mwa wiki na Kamanda wa polisi Mkoa wa Songwe,
Theopista Mallya,wakati akito nasaha zake alipohudhuria ibada ya misa
ya ndoa ya Mkaguzi Msaidizi wa Polisi, Antony Sabasaba, ambaye ni
Msaidizi wa Mkuu wa Kikosi cha usalama barabarani wilaya ya Momba.
Tukio hilo la Sakramenti ya ndoa takatifu lilifanyika
katika kanisa la Katoliki Jimbo Kuu la Mbeya, Parokia ya Mtakatifu Patrick Mjini Vwawa, wilayani Mbozi.
"Kuna
'statement' nimesikia umesema hapo padre kuwa wanandoa wawe tayari
kupokea watoto na kuwalea, huo ni wosia muhimu sana kwani tunapata kesi
nyingi sana za askari kupeleka watoto kwa wazazi wao na kuwatelekeza
bila matunzo".
"
Yaani mzazi amekuzaa, amekulea na kukusomesha hadi umepata kazi kisha
unafunga ndoa na unazaa halafu unampelekea mtoto akulele... hapa hilo
halikubaliki na mimi nitalisimamia na kuchukua hatua" alitahadharisha
Kamanda Mallya.
Pia,
amewataka askari kuwa mfano bora kwenye jamii kwa kuimarisha malezi ya
familia zao ili kuwa na familia zenye kuchukia uharifu.
Aidha, Kamanda Mallya ameiasa jamaii kuwa na utaratibu wa kuwa karibu na familia zao ili kuimarisha malezi ya watoto hali ambayo itasaidia kupunguza vitendo vya ukatili kwa watoto na kuwaepusha kujiingiza kwenye uharifu.
No comments:
Post a Comment