HABARI MSETO (HEADER)


 


Breaking

January 31, 2024

CCM YAWATAKA VIJANA KUJITOKEZA KUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimewataka vijana kujitokeza wa wingi kugombea nafasi mbalimbali za uongozi huku kikiahidi kuwapa fursa kwa kuwapitisha kwa kuwa wanao uwezo wa kuongoza.

Kauli hiyo ilitolewa jijini Dar es Salaam jana na Makamu Mwenyekiti wa CCM Tanzania Bara, Abdulrahman Kinana katika mkutano mkuu maalumu wa ukaribisho wa wananchama wapya 1,167 wa Seneti ya Vyuo Vikuu wa DIT, CBE, IFM na Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima kutoka tawi la Kibasila, Kata ya Upanga Mashariki.

Kinana alisema Chama kinawategemea vijana kwa kuwa wanayo chachu ya mawazo kwa Chama, hivyo wasifikiri kuwa kuna sehemu nyingine mawazo yatatoka bali watambue kuwa wao ni taifa la leo.

Alisema Chama kinawategemea kwa  ushauri, kujenga hoja na kukosoa, hivyo watambue wao ni watu wa kisasa, wasomi na wanakwenda na kasi ya upatikanaji wa taarifa hususan kupitia mitandao ya kijamii.

"Kutokana na hilo mnao uwezo mkubwa wa kutushauri, kutujenga na kutukosoa, tunakutegemeeni sana, toeni mawazo. mwaka huu tuna uchaguzi wa serikali za mitaa, nawasihi vijana jitokezeni na gombeeni katika nafasi zote," alisema.

Kinana alisema Chama kitafanya  kila linalowezekena kuwapitisha vijana wengi katika nafasi za kugombea kwani yeye na Rais Dk.Samia Suluhu Hassan  watafanya kila jitihada kuwapitisha vijana wengi.

"Nawasihi nendeni mkagombee nafasi zote na Chama tutatoa maelekezo kufanya linalowezekena kuhakikisha vijana wanapewa nafasi nanyi hakikisheni mnakipa ushindi Chama chenu," alisema.

Kinana alisema CCM ni kubwa, hivyo wanapaswa kukilinda, kujipanga, kuweka mikakati na kugawa majukumu.

Alisema yapo mambo yanayochangia kukipa ushindi Chama ukiwemo utekelezaji mzuri wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM, hivyo aliwataka vijana kuchagua viongozi wenye uwezo  na sio wa kubebwa wala kutumia fedha kupata nafasi.

Hata hivyo, alisema Chama kisingependa kupata malalamiko bali kitachagua viongozi kulingana na sifa zao.

Kinana aliahidi kutoa kompyuta, mashine ya kuchapisha na ‘printa’ kwa vijana hao wajitegemee katika seneti yao.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam, Abas Mtemvu alisema ofisi ya Chama mkoa itachamgia sh. milioni mbili katika mfuko wa vijana zitakazosaidia kununua vifaa mbalimbali ambavyo vitawawezesha kujitegemea.


ZUNGU

Naibu Spika wa Bunge, Mussa Zungu na Mbunge wa Ilala alisema  wamepata wananchama wapya, wasomi waliobobea zaidi ya 1,000 na wanatarajia watayasemea mambo mazuri yanayotekelezwa na Rais Dk. Samia Suluhu Hassan.

 

Alisema hatua hiyo inaonyesha jinsi Rais Dk. Samia  anavyofanya vizuri na kugusa nyoyo za Watanzania,  hivyo sasa Ilala wanaanza rasmi ajenda ya Samia ya mwaka 2025 kuleta ushindi.

Alisema wameamua kumbeba na kumtetea kiongozi anayesimamia umoja wa Watanzania na kubeba  kero zao.

"Msibabaishwe wala msidanganywe na wasiokitakia mema Chama chetu na nchi yetu. Jimbo la Ilala tutachangia sh. milioni tano mjisimamia na mikopo  inayotewa na serikali msizubae, ichangamkieni mjiimarishe," alisema.

MPOGOLO

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Edward Mpogolo, alimpongeza Kinana kwa kuwa mlezi mzuri wa vijana na jinsi anavyofanya kazi  anawapa nguvu ya kuendelea kuchapaka kazi.

Alisema hali ya siasa kwa wilaya ya Ilala na Mkoa wa Dar es Salaam ni nzuri, hivyo alishukuru na viongozi wa zuri wa Chama," alisema.


V1

Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Ndg. Abdulrahman Kinana, akisalimia Viongozi na Wanachama alipowasili katika Ukumbi wa Mikutano wa Mwalimu Nyerere katika Mkutano wa Ukaribisho wa Wanachama 1170 wa Matawi ya Seneti ya Vyuo na Vyuo Vikuu katika Vyuo Vya CBE,DIT,IAE Mkoa wa Dar Es Salaam.

V2
  Wanachama na Viongozi Mbalimbali wakiwa katika Ukumbi wa Mikutano wa Mwalimu Nyerere katika Mkutano wa Ukaribisho wa Wanachama 1170 wa Matawi ya Seneti ya Vyuo na Vyuo Vikuu katika Vyuo Vya CBE,DIT,IAE Mkoa wa Dar Es Salaam.

V3
Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mhe. Edward Mpogolo akizungumza na Viongozi na Wanachama  katika Mkutano wa Ukaribisho wa Wanachama 1170 wa Matawi ya Seneti ya Vyuo na Vyuo Vikuu katika Vyuo Vya CBE,DIT,IAE uliofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Mwalimu Julius  Nyerere Mkoa wa Dar Es Salaam.

v4
Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Ndg. Abdulrahman Kinana akikabidhi kadi za CCM kwa  Wanachama   1170 wa Matawi ya Seneti ya Vyuo na Vyuo Vikuu katika Vyuo Vya CBE,DIT,IAE patika Mkutano uliofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Mwalimu Julius  Nyerere Mkoa wa Dar Es Salaam.

V5
Wanachama Wapya wakila Kiapo Cha Chama.

V6
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Dar Es Salaam Ndg. Abasi Mtemvu, akizungumza na Viongozi na Wanachama  katika Mkutano wa Ukaribisho wa Wanachama 1170 wa Matawi ya Seneti ya Vyuo na Vyuo Vikuu katika Vyuo Vya CBE,DIT,IAE uliofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Mwalimu Julius  Nyerere Mkoa wa Dar Es Salaam.

V7
Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Ndg. Abdulrahman Kinana, akizungumza na Viongozi na Wanachama  katika Mkutano wa Ukaribisho wa Wanachama 1170 wa Matawi ya Seneti ya Vyuo na Vyuo Vikuu katika Vyuo Vya CBE,DIT,IAE uliofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Mwalimu Julius  Nyerere Mkoa wa Dar Es Salaam.(Picha na Fahadi Siraji wa CCM)

No comments:

Post a Comment

Pages