HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

June 20, 2024

Benki ya CRDB, Nala wasaini makubaliano ya kibiashara kuimarisha zaidi huduma za kifedha kwa watanzania waishio nje ya nchi

Mkurugenzi wa Wateja wa Awali na wa Kati wa Benki ya CRDB, Bonaventura Paul (kulia) na Mwanzilishi na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Nala, Benjamin Fernandes (kushoto) wakisaini mkataba wa makubaliano ya kibiashara yanayolenga kuimarisha zaidi huduma za kifedha kwa watanzania wanaoishi nje ya nchi ambapo Benki ya CRDB itakuwa ikitoa huduma ya kupokea na kuchakata miamala inayotumwa kutoka nje ya Tanzania kupitia Programu ya Nala kwenda mabenki na taasisi nyingine za fedha pamoja na mitandao ya simu. Hafla hiyomilifanyika Makao Makuu ya CRDB jijini Dar es Salaam.

Mkurugenzi wa Wateja wa Awali na wa Kati wa Benki ya CRDB, Bonaventura Paul (kulia) na Mwanzilishi na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Nala, Benjamin Fernandes (kushoto) wakionesha mkataba waliosaini.
Mwanzilishi na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Nala, Benjamin Fernandes akizungumza wakati wa hafla ya kusaini mkataba wa makubaliano ya kibiashara baina na Benki ya CRDB jijini Dar es Salaam.


Balozi wa Tanzania nchini Uingereza, Mbelwa Kairuki, akizungumza wakati wa hafla ya kusaini mkataba wa makubaliano ya kibiashara baina ya CRDB na Kampuni ya Nala yanayolenga kuimarisha zaidi huduma za kifedha kwa watanzania wanaoishi nje ya nchi.

Mkurugenzi wa Wateja wa Awali na wa Kati wa Benki ya CRDB, Bonaventura Paul, akitoa hotuba yake wakati wa hafla ya kusaini mkataba wa makubaliano ya kibiashara na Kampuni ya Nala yanayolenga kuimarisha zaidi huduma za kifedha kwa watanzania wanaoishi nje ya nchi.


 

 

No comments:

Post a Comment

Pages