HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

June 26, 2024

Serikali 'yaipiga Jeki' NHIF kufikisha elimu kwa Umma

Mkuu wa Wilaya ya Ubungo, Hassan Bomboko, akitoa hotuba yake wakati wa kufungua rasmi kituo cha kutoa elimu ya kujiunga na Mfuko wa Taifa ya Bima ya Afya (NHIF) iliyokwenda sambamba na upimaji wa afya bure katika kituo cha mabasi cha kimataifa cha Magufuli jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Meneja wa NHIF Mkoa wa Kinondoni, Dk. Raphael Mallaba.  (Na Mpiga Picha Wetu).
Meneja wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) Mkoa wa Kinondoni, Dk. Raphael Mallaba, akizungumza wakati wa ufunguzi wa kituo cha kutoa elimu ya kujiunga na Mfuko huo iliyokwenda sambamba na upimaji wa afya bure katika kituo cha mabasi cha kimataifa cha Magufuli jijini Dar es Salaam.

 



 
Na Mwandishi Wetu


Serikali imesema upo umuhimu wa kuuongezea nguvu Mfuko wa Afya Bima ya Afya wa NHIF ili uweze kufikisha elimu kwa umma juu ya faida za kuwa na bima ya afya kwa maslahi mapana ya mtanzania mmoja mmoja na taifa kwa ujumla.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mhe; Hassan Bomboko wakati wa ufunguzi wa kituo cha kutoa elimu katika kituo cha mabasi cha kimataifa Mgafuli kilichopo mbezi jijini Dar es Salaam.

"Sisi kama serikali tumeona upo umuhimu wa kuwapa nguvu NHIF kufikisha elimu kwa umma na nitumie hadhara hii kutoa maelekezo kwa watendaji wa kata na mitaa, kwamba kwenye mikutano yote ya hadhara wawape elimu wananchi juu ya umuhimu wa mfuko wa NHIF kwa wananchi wetu, 

"Iwe ajenda, na kaimu afisa tawala uko hapa, magavana wote muifanye hii kazi ya kuhakikisha katika ziara zenu mikutano yenu ya kuwaelewesha wananchi kwamba dunia ya sasa inakuhitaji kuwa na bima ya afya ili uweze kupata huduma kirahisi pasi na kulazimika kutumia pesa ambayo hukuwa umepanga kuitumia .

Japo la pili wananchi tuwe na utamaduni wa kupima afya zetu, leo nimekuta hapa zoezi linaendelea na ni zoezi zuri lialofanywa na wenzetu wa Kairuki nawapongezeni sana, wananchi wetu wamepata huduma hapa na ni huduma ambayo wameipata bila malipo yoyote kwaiyo tunawashukuruni na mfikishe shukrani zetu kwa wakurugenzi na nyie ambao mko hapa kuendesha zoezi hili.

Ilani ya Chama cha Mapinduzi imeelekeza kwamba wananchi wapate elimu juu ya namna ya kujiunga katika bima ya afya, mzifikie na shule zetu za msingi na sekondari muwape elimu wanafunzi na wazazi juu ya faida ya kujiunga na mifuko ya bima ya afya."amesema Bomboko

Niwapongeze sana NHIF kwa kutoa huduma na kuwafikia wananchi wengi. Wananchi wamekuwa wakipatiwa huduma mbalimbali jambo la msingi ambalo limekuekuwa likiendelea ni NHIC kuona ipo haja Serikali kuwa na kituo hapa  katika wilaya yetu ya ubungo. 

Toka kituo hiki kimefunguliwa kimekuwa  na mafanikio makubwa sana nje na utaratibu wa kawaida kimewafikia watu wengi sana na kuwapa elimu na hii elimu ndiyo imewaondoa wasiwasi wananchi  kwamba tunatoa hela lakini yawezekana ni siumwe mimi nikakaa muda mrefu na hela yangu ikaenda bura, lakini leo wamejua umuhimu wa jambo hili.

Amewataka wananchi kutambua kuwa sio lazima hadi uumwe ndio uende hospitali, bali kila mwananchi anaowajibu wa kwenda hospitali kuangalia afya yako na kuweza kujua hali yako kuliko kusubiri kuugua ndio unakwenda hospitali kwani itakusaidia kujua nini ufanye ili afya yako iendeleeee kuwa bora"amesema Bomboko.

"Wananchi wengi walikuwa wanakuja maofisini kwa ajili ya kupima afya zao na changamoto ya wanaokuja maofisini wengi wanakuwa ni wagonjwa. hivyo kama taasisi tumekuwa na mikakati ya kuwafuata huko waliko hapa ni sehemu moja wapo tu lakini tunatembelea kila maeneo ambayo  yana makundi ya wananchi ili tuwape elimu na wananchi wanapojiunga inarahisha kuwafikia kwa kiasi kikubwa zaidi. Hivyo muamko umeendelea kuwepo ndio maana hapa tulipo leo mtashuhudia wananchi wakijaza fomu na kupata bima zao." amesema Meneja wa NHIF Mkoa wa Kinondoni, Dk. Raphael Mallaba.


No comments:

Post a Comment

Pages