HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

July 09, 2024

CRDB yaikabidhi milioni 24 timu ya Taifa ya Olympic 2024

 Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Said Shaibu Mussa ameipongeza Benki ya CRDB kwa uamuzi wenu wa kufanya CRDB Bank Marathon katika nchi tatu kwa maana ya Tanzania, Burundi na DRC.

Balozi Mussa amesema uamuzi huo unaenda sambamba na jititihda zinazofanywa na Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kuifungua nchi na kuboresha mahusiano ya kidiplomasia na jirani zetu.

“Hivyo tunapoona taasisi binafsi kama Benki ya CRDB mkipita katika njia hizo hizo kwa kutoishia kukuza biashara zenu nje ya mipaka bali kuangalia namna gani mnaweza kugusa maisha ya watu katika nchi hizo, tunapata faraja na kuona somo la Dkt. Samia limeeleweka vyema na linatekelezwa kwa vitendo. Hongereni sana,” awesema Balozi Mussa.

Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Bank Group, Abdulmajid Nsekela amesema upanuzi wa CRDB Bank marathon katika nchi za DRC na Burundi unenda sambamba na malengo ya benki ya kujitanua kikanda na kuchochea maendeleo barani Afrika.

Nsekela amesema, Benki ya CRDB imejipanga kikamilifu kusaidia kuweka mazingira wezeshi na kuwawezesha Wananchi katika nchi inapotoa huduma kunufaika na fursa malengo ya Afrika Tuitakayo “The Africa We Want” 2063.

Nsekela amesema mafanikio ambayo Benki ya CRDB imeyapata katika nchi za DRC na Burundi yanatokana na mahusiano mazuri baina ya Tanzania na nchi hizo yakichagizwa na uongozi mahiri wa Rais wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Burundi Evarist Ndayishimye, na Rais wa DRC Congo chini ya Mhe. Rais Félix Tshisekedi.

Katika utekelezaji wa mpango wake wa uwezeshaji kwa vijana kupitia CRDB Bank Marathon, Benki ya CRDB kupitia Taasisi yake ya CRDB Bank Foundation imekabidhi msaada wa fedha kwa timu ya Taifa ya Olympic kushiriki katika Mashindano ya Olympic yatakayofanyika Paris, Ufaransa kuanzia tarehe 26 Julai hadi 11 Agosti 2024, na leo hii tutawakabidhi hundi ya ufadhili.

Akikabidhi mfano wa hundi kwa Makamu wa Rais wa Shirikisho la Riaadha Tanzania, William Kallagjhe, Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Bank Group, Abdulmajid Nsekela amesema uwezeshaji wa timu hiyo ya Taifa ya Olympic kwa vijana wanaokwenda kushiriki utailetea Taifa heshima, bali pia itawaweka katika ramani ya kimataifa, ikitoa njia ya mafanikio kwa wao binafsi, familia zao na jamii kwa ujumla.

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Said Shaibu Mussa, Balozi wa Burundi nchini Tanzania, Mhe. Leontine Nzeyimana, Mwakilishi wa Balozi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) nchini, Patrice Tshekoya na Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Bank Group, Abdulmajid Nsekela wakikabidhi bendera za Tanzania, Burundi, na DRC kwa Jeshi la Kusambaza Tabasamu (JLKT) la CRDB Bank Marathon kama ishara ya kulipa idhini jeshi hilo kusambaza tabasamu katika nchi hizo.


Malengo msimu wa tano wa CRDB Bank Marathon ni kusajili wanajeshi wa kusambaza tabasamu (washiriki) zaidi ya 8,000 na kukusanya zaidi ya shilingi bilioni 2. Katika msimu huu, CRDB Bank Marathon inatarajia kuanzia jijini Lubumbashi nchini DRC Agosti 4 kisha tutaelekea jijini Bunjumbura nchini Burundi Agosti 11 kabla ya kurudi hapa Dar es Salaam Agosti 18.

Balozi wa Burundi nchini Tanzania, Mhe. Leontine Nzeyimana ameipongeza Benki ya CRDB kwa kuanzisha CRDB Bank Marathon nchini humo akisema mbio hizo zitakwenda kusaidia kujenga utamaduni kwa wananchi kujitoa kwa ajili ya kusaidia wenye uhitaji, pamoja na kuchangia maendeleo katika sekta za msingi kama afya.

Balozi Nzeyimana amesema kutokana na umaarufu wa CRDB Bank Marathon kimataifa anategemea kuona mbio hizo kusaidia kuitangaza nchi ya Burundi kote duniani. Balozi huyo ametoa rai kwa watu wa Burundi kujisajili kushiriki mbio hizo huku akiwakaribisha washiriki kutoka Tanzania na nchi nyengine kwenda kushiriki katika mbio zitakazo fanyika tarehe 11 Agosti 2024.

Akizungumzia mchango wa Benki ya CRDB katika uchumi wa nchi hiyo, Balozi Nzeyimana ameishukuru Benki kwa mchango wake katika kusaidia kukuza ujumuishi wa kifedha na kiuchumi nchini Burundi, huku akiitaja kama moja ya mshirika wa kimakakti wa Serikali ya nchi hiyo. Pia alitumia fursa hiyo kuipongeza Benki ya CRDB kwa kuwa benki kiongozi kwa faida ikiwa ni miaka 12 tu toka kuiangia nchini humo.


Mwakilishi wa Balozi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) nchini, Patrice Tshekoya amesifu jitihada za Benki ya CRDB katika kusaidia kutatua changamoto zinazoikabili jamii. Balozi huyo amesema licha ya muda mfupi toka kuingia kwa Benki nchini DRC imeonyesha mfano ambao unapaswa kuigwa na taasisi nyingi wa kujielekeza katika kusaidia changamoto zinazoikabili jamii.

Balozi Masala ameihakikishia Benki ya CRDB uungwaji mkono kutoka kwa Serikali pamoja na WaCongo wote katika mbio hizo akisema ni utamaduni mpya ambao utakwenda kusaidia watu kuwa na mtindo bora wa maisha, pamoja na kujenga uzalendo wa kujitolea kwa ajili ya jamii, na Taifa kwa jumla.

Balozi huyo pia alitoa rai kwa watu wa Congo kujisajili kushiriki mbio hizo huku akiwakaribisha washiriki kutoka Tanzania na nchi nyengine kwenda kushiriki katika mbio zitakazo fanyika tarehe 1

Malengo ya msimu wa tano wa CRDB Bank Marathon ni kusajili wanajeshi wa kusambaza tabasamu (washiriki) zaidi ya 8,000 na kukusanya zaidi ya shilingi bilioni 2. Katika msimu huu, CRDB Bank Marathon inatarajia kuanzia jijini Lubumbashi nchini DRC Agosti 4 kisha tutaelekea jijini Bunjumbura nchini Burundi Agosti 11 kabla ya kurudi hapa Dar es Salaam Agosti 18.

Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Bank Foundation ambaye ndiye Kamanda wa Jeshi la Kusambaza Tabasamu (JLKT) la CRDB Bank Marathon amesema mbali na makundi ambayo yamekuwa yakinufaika na mbio hizo mwaka huu katika kuendeleza azma yetu ya uwezeshaji kwa vijana sehemu ya fedha zitakazokusanywa zitakwenda kusaidia jitihada za kuwajengea uwezo vijana nchini (capacity building).

Katika ripoti iliyowasilishwa na Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Bank Foundation ambaye ndiye Kamanda wa Jeshi la Kusambaza Tabasamu (JLKT) la CRDB Bank Marathon aliyoiwasilisha wakati wa uzinduzi wa msimu wa tano ambapo mbio zetu zinavuka mipaka hadi DRC na Burundi amesema;

Katika misimu minne iliyopita CRDB Bank Marathon imekusanya Shilingi bilioni 2.7 ambazo zilielekezwa katika kusaidia upasuaji kwa watoto zaidi 300 wenye maradhi ya moyo Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), wakinamama wenye ujauzito hatarishi zaidi 150 Hospitali ya CCBRT, Ujenzi wa Kituo cha Mawasiliano Taasisi ya Kansa ya Ocean Road (ORCI), ujenzi wa Kituo cha Afya ya Mama na Mtoto Zanzibar, na kampeni ya utunzaji mazingira ya ‘Pendezesha Tanzania’.

 

 

No comments:

Post a Comment

Pages