HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

February 07, 2013

Flaviana aendelea kuula Majuu


Na Mwandishi wetu
Mwanamitindo wa kimataifa kutoka nchini Tanzania Flaviana Matata ameshiriki katika kampeni za matangazo makubwa ya makampuni ya nguo ya Diesel na  Edun.
 Kampeni hiyo inayoitwa Diesel + Edun ilianzishwa mwaka jana mwezi wa kwanza ambapo muanzilishi wa kampuni hiyo, Renzo Rosso - na waanzalishi wa kampuni ya Edun ,  Ali Hewson na Bono walisafiri nchi za Uganda na Mali na kukutana na wakulima wa pamba barani Afrika.
Waanzilishi hao waliingia makubaliano ya kutengeneza nguo maalum zitakazotokana na pamba ya wakulima hawa wa Afrika na hivyo kuwanufaisha moja kwa moja. Hivyo basi nguo hizi zinatangazwa kama kampeni ili kunufaisha bara la Afrika.
Nguo hizo zitaanza kupatikana mwanzoni mwa mwezi wa tatu katika maduka mbalimbali nchini Marekani na duniani. Pia nguo za Diesel + Edun zitauzwa kupitia mitandao mbalimbali.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Compass Communications Limited, Maria Sarungi Tsehai amesema kuwa Flaviana ambaye aliwahi kuwa Miss Universe Tanzania 2007 anabaki kuwa mwanamitindo pekee kutoka bara la Africa katika kushiriki katika kampeni za nguo hizo.

No comments:

Post a Comment

Pages