HABARI MSETO (HEADER)


 


Breaking

July 12, 2026

CRDB Bima Yazindua Kampeni ya Elimu

Mkurugenzi wa CRDB Insurance, Wilson Mnzava (katikati), akimkabidhi mfano wa hundi Msanii wa Filam, Hamisa Mobeto, wakati akitangwa kuwa baozi wa mfuko huo jijini Dar es Salaam kulia nio meneja wa msanii huyo, Noel Mangoma, kushoto ni Mkuu wa Kitengo cha Uendeshaji wa mfuko huo, Eliam Mosby, waili kushoto ni Mkuu wa kitengo cha Fedha wa Insurance, Tausi Malekano.

2
Mkurugenzi wa CRDB Insurance, Wilson Mnzava (kushoto), akimkabidhi mfano wa hundi Msanii wa Filam, Hamisa Mobeto, wakati akitangwa kuwa baozi wa mfuko huo jijini Dar es Salaam.



Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam


KAMPUNI ya Bima ya CRDB imezindua kampeni maalumu ya kutoa elimu kwa wananchi kuhusu umuhimu wa bima, ikihamasisha jamii kutambua kuwa kinga ni bora kuliko tiba kwa kulinda maisha na mali zao mapema.

Akizungumza jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Bima ya CRDB, Wilson Mzava, alisema kampeni hiyo inalenga kuongeza uelewa wa wananchi kuhusu usalama, uwajibikaji na umuhimu wa kujiandaa mapema kwa kulinda mali na maisha kupitia huduma za bima.

Mzava alisema mbali na kutoa elimu, kampeni hiyo pia inalenga kujenga uhusiano wa karibu kati ya wananchi na huduma za bima kwa kuzungumzia changamoto na hali halisi wanazokutana nazo katika maisha yao ya kila siku.

Aidha, Kampuni ya Bima ya CRDB imemtambulisha mfanyabiashara na msanii Hamisa Mobetto kuwa balozi wa kampeni hiyo, ambapo atashiriki kufikisha elimu ya bima kwa umma na kuhamasisha wananchi kutumia huduma hizo kwa ajili ya kujikinga na majanga mbalimbali.

No comments:

Post a Comment

Pages