HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

July 21, 2013

ZIARA YA WAZIRI MKUU MKOANI RUVUMA

 Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akisalimiana na baadhi ya wafanyakazi wa  Idara ya uhamiaji wakati alipowasili kwenye jengo la Idara hiyo mjini Songea kuweka jiwe la msingi akiwa katika ziara ya mkoa wa Ruvuma Julai 20, 2013. (Picha na Ofisi ya Waziri  Mkuu)
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akikagua mabwawa ya kufugia samaki wakati alipotembelea Kituo cha Maendeleo  ya Ufugaji Samaki cha Ruhila kilichopo mjini Songea. Alikuwa katika ziara ya mkoa wa Ruvuma.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akitazama chakula cha samaki wakati alipotembelea Kituo cha Maendeleo  ya Ufugaji wa Samaki cha Ruhila kilichopo Songea Mjini akiwa katika ziara ya mkoa wa Ruvuma Julai 20, 2013. Wapili kulia ni mkewe, Mama Tunu Pinda na Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Thabit Mwambungu.
 Waziri Mkuu, Mizengo Pinda  na mkewe Tunu (kushoto kwake) wakitazama ngoma ya wanawake wa Songea kabla ya kuhutubia mkutano wa hadhara mjini Songea.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akisalimiana na wanafnzi wa Shule ya Sekondari ya Songea Girls baada ya kuhutubia mkutano wa hadhara mjini Songea Julai 20, 2013. Alikuwa katika ziara ya mkoa wa Ruvuma. 
Baadhi ya Waislam walioalikwa katika futari iliyoandaliwa na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda kwenye Ikulu ndogo ya Songea wakishiriki katika futari hiyo.
Mke wa Waziri Mkuu, Mama Tunu Pinda  (wapili kulia)  akizungumza na baadhi ya wanawake  walioshiriki katika futari ambayo Waziri Mkuu, Mizengo Pinda aliwaandalia baadhi ya Waislam wa Songea. 

No comments:

Post a Comment

Pages