HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

September 10, 2014

WAREMBO WA REDDS MISS TANZANIA 2014 KUINGIA KAMBINI TAREHE 13 SEPTEMBA 2014

Washiriki wa Fainali za Mashindano ya urembo ya Redds Miss Tanzania 2014 kutoka mikoa mbalimbali nchini wataanza kambi rasmi ya mafunzo kwa kuingia kambini Jumamosi ya tarehe 13 Septemba 2014.
 
Washiriki hao 30  watapiga kambi  katika Hotel ya JB Belmont iliyopo katikati ya jiji ya D’salaam ambapo mazoezi na mafunzo ya aina mbalimbali yatatolewa kwa muda wa wiki nne kabla ya Fainali za Taifa ambazo zimepangwa kufanyika mapema mwezi ujao.
 
Wakiwa kambini warembo hao watapewa semina kuhusu masuala mbalimbali yanayohusu  mashindano ya urembo, kusaini Mikataba n.k.
 
Kwa mujibu wa Ratiba ya Kambi iliyotolewa na Lino International Agency Limited, waandaji wa Mashindano ya urembo ya Miss Tanzania, washiriki hao watakuwa hotelini hapo kwa muda wa siku 3 tu, na baadaye kuanza ziara ya kutembelea Vivutio mbalimbali  vya Utalii katika mikoa ya Morogoro, Tanga, Kilimanjaro, Manyara na Arusha.
 
Washiriki hao watarejea jijini D’salaam tarehe 28 Septemba 2014 na kufikia katika hotel ya Kijiji Beach  Kigamboni na kuendelea na ratiba yao  ya mafunzo  kama ilivyopangwa na waandaji.
 
Orodha ya washiriki pamoja na mikoa wanayowakilisha imeambatanishwa.
Shindano la Redds Miss Tanzania linadhaminiwa na REDDS ORIGINAL.

No comments:

Post a Comment

Pages