HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

March 02, 2015

Omog,Shikanda watimuliwa rasm Azam FC

Aliyekuwa Kocha wa Azam FC, Joseph Omog.

NA KOKUJUNA KATAMA

KOCHA Mkuu wa Klabu ya Azam FC Joseph Omog na Msaidizi wake Ibrahim Shikanda, wametimuliwa rasm kuinoa timu hiyo kutokana na kushindwa kutimiza matakwa ya mkataba wao.

Habari ambazo Habari Mseto imezipata hivi punde, kocha huyo na msaidizi wake wametimuliwa kutokana na kukiuka kipengele cha kuipeleka timu hiyo katika hatua ya makundi ya michuano ya Kimataifa ambapo Azam FC ambao ni Mabingwa watetezi Ligi Kuu Tanzania Bara waliondolewa na El Merreikh kwa kubugizwa mabao 3-2 baada ya nyumbani kushinda 2-0 huku ugenini wakichapwa bila huruma 3-0.

Hata hivyo Mtendaji Mkuu wa klabu hiyo Saad Kawemba alithibitisha kutimuliwa kwa makocha hao, na kusema kuwa, wamekiuka masuala ya kimkataba.

“Tumevunja mikataba yao, na mazungumzo tumeyafanya, na kukubaliana, hivyo basi hakuna wa kumlaum mwenzake kwani wao wamekiuka mkataba,”alisema na kuongeza kuwa George Nsimbe ndiye atainoa timu hiyo mpaka ligi kumalizika.



Kutokana na timua timua hiyo nafasi ya Mcameroon huyo inatarajiwa kuzibwa na aliyekuwa Kocha Mkuu wa Simba Patric Liewig.

No comments:

Post a Comment

Pages