HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

February 17, 2017

RED CROSS YAKABIDHI KADI ZA UANACHAMA IDARA YA MAAFA

Rais wa Chama cha Msalaba Mwekundu Tanzania Bw. Mwadini Jecha (katikati) akiweka saini kitabu cha wageni Idara ya Uratibu wa Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu walipotembelea Idara hiyo na kukabidhi Kadi za Uanachama kwa Idara  hiyo.
Mkurugenzi wa Chama Cha Msalaba Mwekundu Tanzania Bw.Renatus Mkaruka (wa kwanza kulia) akizungumza jambo wakati wa zoezi la kukabidhi kadi za Uanachama wa chama hicho kwa Idara ya Uratibu wa Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu.
Mkurugenzi wa Idara ya Uratibu wa Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu Brig. Jenerali Mbazi Msuya (kulia) akipokea kadi ya uanachama wa Chama cha Msalaba Mwekundu Tanzania kutoka kwa Rais wa Chama hicho Bw. Mwadini Jecha.
Mratibu wa Maafa Idara ya Uratibu wa Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu Bw.Charles Msangi akipokea kadi ya uanachama wa Chama cha Msalaba Mwekundu Tanzania kutoka kwa Katibu wa chama hicho Bw. Julius Kejo katika Ofisi za Idara hiyo Dar es Salaam.
(PICHA ZOTE NA OFISI YA WAZIRI MKUU)

No comments:

Post a Comment

Pages