Mtaalam kutoka Taasisi ya TABIO, Abdallah Mkindi akifafanua jambo
katika warsha ya siku moja iliyoshirolikisha wanaharakati wanaopinga
Teknolojia ya Uhandisi Jeni (GMO), wakulima wa kilimo hai, waandishi wa
habari na wataalam kutoka Serikalini.
Washiriki wa warsha kuhusu madhara ya GMO wakimfuatilia mtoa mada.
Muandaaji wa warsha kuhusu madhara ya GMO, Austin Makani akifafanua jambo mbele ya washiriki wa warsha hiyo. NA SULEIMAN MSUYA
KATIKA
kuhakikisha nchi ya Tanzania haingii katika mtego wa matumizi ya bidhaa
zinazotokana Teknolojia ya Uhandisi Jeni (GMO) wanadau wameshauri
kuwepo na mjadala wa kitaifa na kutolewa elimu kuanzia shule ya msingi
kuhusu madhara yake.
Wadau hao wanakuja na ushauri huo ambapo kwa sasa dunia nzima pamoja na kuwepo mikataba, sheria, kanuni na miongozo ya uzalishaji na matumizi ya bidhaa hizo wanapiga vita kwa kile kinachodaiwa bidhaa za GMO kuwa na madhara kwa viumbe hai.
Wakichangia kwenye warsha ya siku moja iliyofanyika jijini Dar es Salaam na kushirikisha wakulima wa kilimo hai na wanaharakati wanaopambana na matumizi ya GMO wadau hao walisema mapambano dhidi ya bidhaa hizo yanahitaji elimu na mjadala wa kitaifa.
Abdallah Mkindi kutoka Tanzania Alliance for Biodiversity (TABIO), alisema kuruhusu GMO nchini ni kurudisha nyuma mkulima kwa kuwa mbegu hizo sio endelevu.
Alisema wanatarajia mwishoni mwa mwaka huu jijini Dodoma wataandaa tukio ambalo litajikita kwenye kuzungumzia chakula na mbegu ili kusaidia jamii kuelewa kwa kina madhara ya GMO.
Wadau hao wanakuja na ushauri huo ambapo kwa sasa dunia nzima pamoja na kuwepo mikataba, sheria, kanuni na miongozo ya uzalishaji na matumizi ya bidhaa hizo wanapiga vita kwa kile kinachodaiwa bidhaa za GMO kuwa na madhara kwa viumbe hai.
Wakichangia kwenye warsha ya siku moja iliyofanyika jijini Dar es Salaam na kushirikisha wakulima wa kilimo hai na wanaharakati wanaopambana na matumizi ya GMO wadau hao walisema mapambano dhidi ya bidhaa hizo yanahitaji elimu na mjadala wa kitaifa.
Abdallah Mkindi kutoka Tanzania Alliance for Biodiversity (TABIO), alisema kuruhusu GMO nchini ni kurudisha nyuma mkulima kwa kuwa mbegu hizo sio endelevu.
Alisema wanatarajia mwishoni mwa mwaka huu jijini Dodoma wataandaa tukio ambalo litajikita kwenye kuzungumzia chakula na mbegu ili kusaidia jamii kuelewa kwa kina madhara ya GMO.
Mkindi
alisema TABIO imekuwa ikishirikiana na mashirika ya ndani na nje
kuhakikisha wakulima wanazingatia kilimo hai ambacho kinatumia mbegu
asili na kuachana na mbegu ambazo sio za kudumu.
"Sisi
TABIO tumedhamiria kushirikiana na Serikali na wadau wengine
kuhakikisha GMO haingii nchini kwa njia yoyote kwani ushahidi upo kuwa
bidhaa na mbegu zake zina madhara kwa binadamu na viumbe hai wengine,"
alisema.
Alisema hoja ya
watu wa GMO imejikita katika ukame, wadudu vamizi na mabadiliko ya tabia
nchi hali ambayo inaweza kudhibitiwa kwa kuwepo elimu ya kutunza mbegu
asili kama ilivyokuwa zamani na kuhamasisha utunzaji mazingira.
Mwakilishi
kutoka Kundi la Kupinga Matumizi ya GMO Tanzania, Albert Kamala alisema
iwapo hakutakuwa na kauli moja baina yao kuna dalili ya jamii kuangamia
siku chache zijazo.
Kamala
alisema wao wameamua kupinga GMO kwa kuwa wanajua na kuona madhara yake
kuanzia shambani hadi majumbani hivyo wanaamini Serikali inapaswa
kuunga mkono kwa nguvu zote ili utekelezaji uonekane.
"Tumeamua
kuwakutanisha hapa leo ili tuweze kuzungumza lugha moja kati ya sisi
wanaharakati wa kupinga GMO na wakulima na baadae tupeleke ujumbe mmoja
Serikalini ili hatua zichukuliwe kwani dalili sio nzuri iwapo tutaruhusu
kilimo na matumizi ya bidhaa hizo katika nchi," alisema.
Naye
Sabrina Masinjila alisema utafiti unaonesha kuwa mbegu za GMO
zimeendelea kuwa na athari zaidi kuliko faida kwa wakulima hivyo
zinapaswa kupingwa kila mahali.
"Inasemekana
mbegu hizo zinaimarisha wadudu vamizi, lakini kilimo hicho kinataka
nafasi sana jambo ambalo ni changamoto kwa wakulima wadogo hata huko
katika nchi ambazo zilianza zimeanza kuacha kwani hasara ni kubwa
zaidi," alisema.
Aidha,
alisema taarifa mbalimbali zinaonesha kuwa mazao yatokanayo na GMO
yamekuwa yakichangia ongezeko la saratani duniani hivyo hakuna sababu ya
kuunga mkono.
Masanjila
alisema Tanzania inapaswa kuwa na mjadala wa kitaifa ambao utatoa
muongozo wa nini cha kufanyika ili kutoka katika janga hilo.
Bonaventure
Charles Mwanharakati wa kupinga GMO kutoka Arusha aliomba Watanzania
wapaze sauti ili kuhakikisha mbegu NA bidhaa za GMO hazipati nafasi
nchini.
Mwanaharakati
huyo alisema juhudi zielekezwe kwenye matumizi ya mbegu asili ambazo
zinaonesha kuwa na matokeo chanya kwa miaka mingi.
"Pamoja
na kupaza sauti pia kuwepo mashamba darasa ambayo yatasaidia wakulima
kutambua mbegu asili ni zipi na GMO ni zipi kwani wakati mwingine ni
changamoto kutambua," alisema.
Ofisa
Miradi wa Umoja wa Walima Matunda na MbogaMboga Zanzibar (UWAMWIMA)
Khamis Issa Mohammed, alisema mjadala wa kitaifa utasaidia jamii
kutambua thamani ya chakula na mbegu asili kwenye maisha yao tofauti na
ilivyo sasa.
Mohammed
alisema ufanisi wa mjadala huo unatakiwa kuhusisha makundi yote muhimu
ambao ni wakulima, wanaharakati, waandishi wa habari, wanadau wa
maendeleo na Serikali ili kuwa na mtazamo mmoja.
Mwenyekiti
wa Umoja wa Waandishi Mkoani Dar es Salaam (DCPC), Irene Mark alisema
mapambano ya GMO yanaweza kufanikiwa iwapo elimu itatolewa kuanzia elimu
ya msingi.
Aidha
aliwataka wadau kuwatumia waandishi wa habari kuanzia ngazi za awali
katika mapambano hayo na sio kusubiri kuwapa taarifa ya utekelezaji.
"Mimi
naamini mapambano haya yanahitaji kujikita kuanzia elimu ya msingi, ila
naomba msitutumie kuripoti mliochokiona tuwekeni kwenye mipango yenu
kuanzia ngazi ya awali tutafika pamoja," alisema.
Kwa
upande wake Mtafiti wa Kilimo kutoka Taasisi ya Utafiti wa Kilimo (TARI
-Dakawa), John Joseph alisema changamoto ya GMO inahitaji uwanda mpana
wa mjadala ili kuwa kitu kimoja.
Alisema TARI-Dakawa wanaendelea na utafiti wa mbogamboga asili hivyo ni imani yake suluhu ya mbegu zenye mashaka itapatikana.
Akiwasilisha
mada katika warsha hiyo ya siku moja Mwanasheria kutoka Ofisi ya Makamu
wa Rais Muungano na Mazingira, Isakwisa Mwamukonda alitoa rai kwa
wanaharakati wanaopinga GMO kufanya utafiti wa kina kuhusu mbegu na
bidhaa kwa kuwa ina faida na hasara.
Mwamukonda
alisema iwapo bidhaa na mbegu GMO zipo nchini ni wazi kuwa zipo
kisheria kwa kuwa sheria zetu zinaruhusu ila kwa kufuatwa hatua
mbalimbali muhimu.
"Tanzania imesaini mikataba ya kimataifa kama Mkataba wa Bioaniwai (1992), Mkataba Mdogo wa Cartagana (2002), Mkataba wa Nagaya.
Sera
ya Taifa Mazingira (1997), Sera ya Taifa ya Biotechnolojia ya Kisasa
(2009), Sera ya Kilimo ya (2019), Sheria ya Mazingira ya (2004) na
Sheria za Kisekta," alisema.
Mwanasheria
huyo alisema katika kukabiliana na GMO nchini ni lazima wafanye utafiti
wa kina ambao utawezesha watunga sera kuelewa na kufanya maamuzi
sahihi.
Mmoja wa
Waandaaji wa warsha hiyo, Austin Makani alisema warsha hiyo imewapa
muongozo wa nini cha kupeleka Serikalini ili hatua stahiki zichukuliwe
dhidi ya hofu ya bidhaa na mbegu za GMO nchini.
"Kwa
ujumla tunashukuru na tumepokea michango yote ambayo imetolewa na
tutahakikisha inafika sehemu husika kwa hatua zaidi," alisema.
No comments:
Post a Comment