HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

May 13, 2013

TUICO yakabidhi cheti, rambirambi familia ya Tandau

 Katibu mkuu Taifa wa  Chama cha Wafanyakazi wa Viwanda, Biashara, Taasisi za Fedha, Huduma na Ushauri (TUICO),Boniface Nkakatisi, akimpa pole mjane wa marehemu balozi Alfred Tandau, Margareth Tandau, kwa niaba ya chama hicho,  wakati alipofika nyumbani kwake Magomeni jijini Dar es Salaam jana  kutoa salamu za rambirambi sanjari na kuikabidhi familia hiyo kwa niaba ya marehemu cheti cha cha uanachama wa heshima alichotunukiwa na mkutano mkuu wa chama hicho mnamo April 19, mwaka huu.
Katibu Mkuu Taifa wa  Chama cha Wafanyakazi wa Viwanda, Biashara, Taasisi za Fedha, Huduma na Ushauri (TUICO), Boniface Nkakatisi, akimpa pole sambamba na kumkabidhi cheti cha uanachama wa heshima kwa niaba, mjane wa marehemu balozi Alfred Tandau, Margareth Tandau,  wakati alipofika nyumbani kwake eneo la Magomeni, jijini Dar es Salaam jana,  kutoa salamu za rambirambi sanjari na kuikabidhi familia hiyo kwa niaba ya marehemu cheti cha cha uanachama wa heshima, alichotunukiwa na mkutano mkuu wa chama hicho mnamo April 19, mwaka huu, kwa kutambua mchango wake.

Na Mwandishi Wetu

Uongozi wa Chama cha Wafanyakazi wa Viwanda, Biashara, Taasisi za Fedha, Huduma na Ushauri (TUICO), kimejumuika na familia ya aliyekuwa mwanachama wa chama hicho, marehemu Alfred Tandau kwa lengo la kutoa salamu za rambirambi zilizokwenda sambamba na kuikabidhi familia hiyo cheti cha cha uanachama wa heshima, kwa niaba ya marehemu.

Mapema Aprili 19, mwaka huu, Mkutano Mkuu wa TUICO Taifa, uliwatunuku waliokuwa wanachama wake sita vyeti vya heshima mkoani Morogoro kwa kutambua mchango wao ndani ya chama, akiwemo Tandau, lakini hata hivyo hakuweza kuhudhuria hafla hiyo kutokana na tatizo la kiafya.

Wengine waliotunukiwa vyeti hivyo ni pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, Eng Stella Manyanya (Mb), Felister Bura (Mb), Wakili Julius Bundala, na Zephania Sumbe.

Akizungumza nyumbani kwa marehemu, eneo la Magomeni, Dar es Salaam jana, Katibu Mkuu wa TUICO Taifa, Boniface Nkakatisi, alisema wamepokea kwa mshtuko na masikitiko makubwa taarifa za msiba huo mzito, ambao umeacha pigo kubwa kwa familia na wanachama wote wa chama hicho nchini kote.

“Marehemu alikuwa na mchango mkubwa ndani ya chama enzi za uhai wake, muda mwingi alikuwa karibu yetu, alitushauri mambo mengi kwa ustawi wa chama na wanachama, na ndio sababu mkutano mkuu wa Tuico uliamua kumtunuku cheti cha uanachama wa heshima kama ishara ya kuenzi na kutambua mchango wake,” alisema Nkakatisi.

Aliongeza kuwa Marehemu Tandau alipenda sana kujihusisha na masuala ya vyama vya wafanyakazi, na mara kadhaa amekuwa sehemu ya utatuzi wa kero na migogoro, hususan ile inayohusiana na haki ya msingi ya mfanyakazi.

“Mahusiano na ushiriki kwenye vyama vya wafanyakazi ilikuwa ndio kipaumbele chake..mimi mwenyewe wakati fulani nikiwa mwalimu mkoani Mtwara alikuwa ni miongoni mwa watu walionishawishi kujihusisha na vyama vya wafanyakazi, kama chama tutaendelea kumkumbuka na kumuenzi,” alisema Nkakatisi.

Kwa upande wake, Msemaji wa familia hiyo, Benny Tandau, mbali ya kushukuru uongozi wa chama hicho, alisema marehemu alipenda zaidi kujihusisha na vyama vya wafanyakazi kwa sababu aliamini ndiyo sehemu pekee inayoweza kuunganisha umoja na mshikamano wa nguvu kazi ya mwanadamu katika kufikia haki, usawa na matarajio kwa mustakabali mzuri wa ajira yake.  

No comments:

Post a Comment

Pages